Netanyahu aomba radhi kuuwawa kwa mateka 6

                                    Waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyau  (Picha na DW)

Waziri mkuu  wa Israel  Benjamin Netanyahu ameomba radhi kwa Waisraeli kwa kushindwa kuwarudisha mateka sita waliopatikana wameuwawa huko Gaza,  siku ya jumamosi  .

Kauli yake inakuja  baada ya  maandamano Makubwa ya barabarani  katika miji mbalimbali  ikiwemo Jerusalemu na Tel  Aviv  yakimshinikiza  waziri mkuu Netanyahu kukubaliana na makubaliano  ya Hamas ili  kurejesha mateka 101 waliosalia katika mikono wanamgambo wa  Hamas.

Hata hivyo serikali ya Benjamin Netanyau ilikimbilia mahakamani kupinga maandamano  na Mgomo uliongozwa na chama cha wafanyakazi wa nchi  hiyo ambao ulianza septemba 2, 2024 saa 12: 00 za Asubuhi na kusamba nchi nzima ikiwemo jiji la Jerusalemu na Tel aviv

Wakati mgomo huo wa siku moja ukiendelea, mahakama ikaamuru mgomo huo kusitishwa kwani haukulenga maswala ya uchumi  au utetezi  wa wafanyakazi  kama ulivyo wajibu wa chama cha wafanyakazi .

Wakati hayo yakiendelea huko Israel Uingereza imetangaza itasitisha baadhi ya mauzo ya silaha kwa Israel, waziri wa mambo ya nje David Lammy BBC amesema hayo jumatatu tarehe 2 septemba mwaka huu.

Bw Lammy alisema uamuzi huo unafuatia mapitio ya leseni za mauzo ya silaha za Uingereza, ambayo iligundua kuwa kuna hatari ya wazi kwamba zinaweza kutumiwa kufanya ukiukaji mkubwa wa sheria ya kimataifa ya kibinadamu".

"Ni kwa masikitiko kwamba nalijulisha Bunge leo tathmini niliyoipata inaniacha siwezi kuhitimisha kitu kingine chochote isipokuwa kwamba kwa uuzaji wa silaha za Uingereza kwa Israeli, kuna hatari ya wazi kwamba zinaweza kutumika kufanya au kuwezesha kosa kubwa- ukiukaji wa sheria za kimataifa za kibinadamu."

Post a Comment

0 Comments