Papa Francis alaani mauaji yanayoendelea Lebanon na Israel

 

Kiongozi wa kanisa katoliki Duniani Papa Francis amelaani na kukosoa hali ya machafuko inayoendelea kuongezeka Lebanon akisema kuwa kupitia machafuko hayo Israel imeendelea kuua mamia ya watu kusini mwa Lebanon.

Papa Francis amesema hayo septemba 25,2024 huku akisistiza jumuia ya umoja wa mataifa kufanya juhudi ya kusitisha mgogoro huwo ili kuokoa maisha ya raia wa nchi hizo.

Awali katibu mkuu wa umoja wa mataifa Antonio Gutteres akinukuliwa na DW katika mkutano wa 76 wa umoja wa mataifa uliofanyika New York marekani septemba 24,2024 na kusema watu wa Lebanon, Israel na ulimwengu mzima ni lazima wahakikishe kuwa Lebanon haigeuki na kuwa Gaza nyingine.

Usiku wa septemba 24,2024 Jeshi la Israel (IDF) limekiri na kusema linafanya mashambulizi mengi ya anga kusini mwa Lebanon na katika bonde la mashariki la Bekaa baada ya kundi la Hezbollah kufyatua kombora la masafa marefu hadi mji wa Tel Aviv.


Sehemu ya uharibifu uliotokana na mashambulizi ya Israel nchini Lebanon.(picha na DW)
Kwa upande wa Lebanon kupitia shirika la habari la serikali ya nchi hiyo limeripoti kuwa watu watau wamefariki kufuatia shambulizi la Israel katika kijiji cha Maaysra katika wilaya ya Keserwan kaskazini mwa mji mkuu Beirut.

Shirika la habari la serikali ya Lebanon limeongeza kuwa roketi mbili zimeanguka katika kijiji cha Maaysra, chenye idadi kubwa ya Washia katika eneo la milima la wakristo lililoko Keserwan kiasi cha kilometa 25 kutoka mji mkuu.

Hii ni mara ya kwanza kwa kundi la Hezbollah kudai kufanya shambulizi la kombora la masafa marefu tangu vita vyake na Israel vilipoanza baada ya kundi la Hamas kufanya shambulizi kubwa nchini Israel mnamo Oktoba 7  2023.

Mwandishi; Ramadhan Zaidy

Mhariri; Eunice Jacob

Post a Comment

0 Comments