Rais Samia aagiza usimamizi wa bei elekezi ya mazao.

 

Rais wa Jamuhuri ya muungano wa Tanzania Dkt .Samia Suluhu Hassan ameagiza  uongozi wa wilaya ya Mbinga mkoani Ruvuma kusimamia bei elekezi ya mazao na kutoa  elimu kwa wakulima ili kuwaongezea maarifa ya biashara yenye tija na kuipatia serikali mapato. 

Dkt, Samia amesema hayo septemba 25,2024 ikiwa ni siku ya pili ya ziara  ya kikazi ya siku tano mkoani humo yenye lengo la kukagua miradi ya maendeleo na kuweka mawe ya msingi mkoani Ruvuma.

‘’wakulima wawezeshwe kuuza mazao kwa bei elekezi yenye manufaa ambayo itawapa mapato ya kufuta jasho lao na kuhakikisha wanarudisha gharama walizozitumia kulima na wabakiwe na faida kwaajili ya mahitaji ya familia’’alisema Rais Samia.

Awali Waziri wa kilimo Mhe;Hussein Bashe(Mb) wakati akizungumza na wananchi amesema Serikali itahakikisha inatoa mwongozo wa mbegu za mahindi na kuingiza kwenye mfumo wa ruzuku huku akiahidi kuwachukulia hatua za kisheria wale wanao uza mbegu bandia.

Aidha Mhe; Bashe amesema mbegu hizo zitapatikana kwa namba  wanayotumia wanunuzi wa mbolea ili kuondokana na uhujumu uchumi ndani ya taifa   kwa lengo la wakulima nchini kununua mbengu zilizo kusudiwa kwa  kilimo chenye tija.

‘’Kuanzia sasa mbegu zitakuwa zinauzwa na karatasi maalumu ili mkulima anaponunua mahindi mfuko ule utawekwa namba ya kukwangua kama unavokwangua vocha na kukuletea taarifa  kwenye simu yako moja kwa moja’’alisema Waziri Bashe.



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akizindua Jengo la Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Mbinga mkoani Ruvuma tarehe 25 September 2024 kushoto ni Waziri wa TAMISEMI Mhe: Mohamed Mchengerwa.

Ni ziara ya kwanza ya  kikazi ya  kutembelea na kukagua miradi mbalimbali ya kimaendeleo mkoani  Ruvuma na viunga vyake ambapo  Rais Dkt. Samia Suluh Hasan ameweka mawe ya msingi katika Ghala la nafaka Luhimba,pamoja na uzinduzi wa jengo la ofisi ya Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Mbinga mkoani humo.

Mwandishi; Shukuruimana Revokatus.

Mhariri: Eunice Jacob.

Post a Comment

0 Comments