picha Wizara ya Nishati
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameelekeza Watanzania kunufaika na rasilimali zinazochimbwa katika maeneo yao kwa kutoa fursa mbalimbali ikiwemo ajira. Hayo yameelezwa na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati,
Mhe. Dkt. Doto Biteko Septemba 10, 2024 mkoani Mtwara katika hafla ya kukabidhi
leseni ya uendelezaji wa eneo la ugunduzi wa gesi asilia katika Kitalu cha
Ruvuma, eneo la Ntorya ambapo Shirika la Maendeleo ya Petroli (TPDC) pamoja na
Kampuni za ARA Petroleum Limited na Ndovu Resources Ltd ni wabia.
“ Mhe. Rais alielekeza wananchi waliopo maeneo yenye
rasilimali wanufaike kabla ya maeneo mengine, alitoa kibali cha mradi mkubwa wa
gesi na tutajenga kiwanda cha kuzalisha gesi na kuboresha kituo cha kuzalisha
umeme Songa.” Amesema Dkt. Biteko.
Dkt Biteko amesema katika mradi wa Ntorya vitachimbwa visima namba 1 na 2 pamoja na kujenga bomba la kusafirisha gesi kutoka katika kisima hadi Madimba kilomita 34 na katika kipindi cha miezi sita bomba litakuwa limejengwa.
Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko,katika Halfa ya kukabidhi leseni ya uendelezaji wa Eneo la Ugunduzi wa Gesi la Ntorya .
Kwa upande wake, Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, Mhe. Kilumbe Ng’enda amesema kuwa matumizi ya gesi yamepungua kutokana na ongezeko la umeme katika Gridi ya Taifa hivyo gesi iliyokuwa inatumika kuzalisha umeme itaelekezwa katika matumizi mengine, ambapo zaidi ya asilimia 60 ya umeme uliokuwa unazalishwa awali iiitokana na gesi.
“
Tunatarajia katika ushirikiano huu tutapata faida na kusaidia jamii ya
Mtwara pamoja na kuitambulisha Tanzania huko duniani kama wazalishaji wa gesi,”
ameeleza Balozi huyo.
Mkurugenzi
wa Shirika la Maendeleo ya Petroli (TPDC), Bw. Musa Makame amesema
kuwa mradi huo ulianza kwa kushirikiana kati ya Serikali, TPDC na Kampuni ya
Ndovu Resources.
“
Mwaka 2017 uchimbaji ulifanyika na kupata gesi, hadi sasa tuna futi trilioni
1.6 ambazo zimegundulika na kuhakikiwa, na mwaka huu hadi ujao tunachimba
kisima na tayari tuna visima viwili na tunaenda kuchimba cha tatu,”
amesema Bw. Makame.
Ameongeza
kuwa TPDC inajenga bomba la kusafirisha gesi na kiwanda kidogo cha
kuchakata gesi iwe kimiminika na kupeleka kwenye maeneo ambayo hayajafikiwa na
mabomba na kisha kwenda kwenye maeneo mengine. ,Aidha, Shirika hilo litatoa
fedha kiasi cha shilingi milioni 750 kwa ajili ya kujenga kituo cha afya
ikiwa ni sehemu ya faida ya uwepo wa mradi huo katika eneo hilo.
0 Comments