Kasulu TC wahimizwa kushiriki Uchaguzi serikali za mitaa

 

Msimamizi wa uchaguzi halmashauri ya mji  Kasulu,Mwl. Vumilia Simbeye amewataka  wakazi wa mji wa Kasulu kujitokeza kwa wingi katika zoezi la uandikishaji wa  wapiga kura wa serikali za mitaa unatarajiwa kuanza tarehe 11 hadi 20 Octoba 2024.

 Mwalimu Simbeya  amesema hay oleo  septemba 26,2024 katika kikao na waandhishi wa habari katika ofisi za halmashauri ya mji Kasulu wakati akitoa maelekezo ya kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa kwa mwaka 2024.

“Maelekezo haya nayatowa siku 62 kabla ya uchaguzi kwa lengo la kuhakikisha kuwa kila mgombea pamoja na wapiga kura wanapata haki  na uchaguzi unafanyika kwa uwazi na usawa kwa kuzingatia sheria na taratibu zilizowekwana serikali” Amesema Mwalimu Vumilia.

Aidha Mwalimu Vumilia ameongeza kuwa kabla ya  kuanza zoezi la uandikishaji   Octoba 11, mwaka huu wananchi watapewa maelekezo ya vituo  vya kujiandikisha  katika mitaa yao .

“tarehe 1 hadi 7 mwezi novemba zitakuwa siku za kuchukua fomu za wagombea kwa wananchi  wenye sifa, wkati huo tarehe 11 hadi 20 zoezi la uandikishaji litakuwa linaendelea na kampeni zitaanza novemba 20 hadi 26 ,Ambapo   tarehe 27  novemba mwaka huu  utafanyika uchaguzi wa serikali za mitaa” Amesema Mwalimu Vumilia.

Nao  baadhi ya  wananchi katika halmashauri ya mji Kasulu wamesema kuwa wamejipanga vilivyo kuelekea uchaguzi huo, huku wakihimiza uchaguzi wa kidemokrasia kwa wagombea na wasimamizi wa ucahaguzi  ili kulinda amani ya eneo husika.

“tumejipanda vilivyo kuelendea uchaguzi wa serikali za mitaa katika maeneo yetu lakini pia niiombe selikali kuzingatia demokrasia ili kulinda amani na utulivu wa mji wetu” wamesema Baadhi ya wananchi.



Mchungaji kiongozi wa kanisa la anglikana na mwenyekiti wa baraza la cct kasulu mji        Mch. Asheri Mageje (picha na Elukaga  kyusa )

        

Kwa upande wa viongozi wa dini  Kasulu ,wakiwakilishwa na Mchungaji Kiongozi Kanisa la Anglican Wilaya ya Kasulu mji  na mwenyekiti Baraza la Kikristo Tanzania  (CCT) Wilaya ya  Kasulu mji Asheri Mageje amewahimiza wanasiasa kutunza Amani,Haki na uadilifu wa kila mwananchi .

“Nawashukuru viongozi wa Halmashauri kwa kuwashirikisha wananchi kuelekea uchaguzi waserikali za mitaa ,Pia  Nawaomba Wanasiasa tulinde Amani ya mji wetu Kasulu tunapoelekea Zoezi la uandikishaji ,kampeni na  uchaguzi Serikali ili kila mwananchi apate haki yake kisheria “

Uchaguzi wa serikali za mitaa hufanyika kila baada ya miaka mitano ambapo wananchi huchagua serikali itakayo waoongoza wananchi wa mtaa husika katika kipindi cha miaka mitano ambapo uchaguzi wa serikali za mitaa uliopita ulifanyika Novemba 2019.

Post a Comment

0 Comments