Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt, Samia Suluhu Hassani amewataka wananchi
kujitokeza kwa wingi katika uchaguzi wa serikali za mitaa ili kuchagua viongozi
sahihi kwa maendeleo ya nchi .
Rais Samia ameyasema hayo leo Septemba 26 Wilayani ya Namtumbo Mkoani Ruvuma alipokuwa
akizungumza na wananchi na kusisitiza kuwa Ushiriki wa kutosha
wa wanachi katika kuchagua viongozi bora wa serikali za mitaa unawashirikisha Katika kuleta maendelo ya nchi.
“Mwanachi anawajibu wa kuchangua viongozi bora, hili
ni jukumu la kila Mtanzania hivyo
tujitokeze kwa wingi ili kufanya maamuzi yaliyo sahihi ’’Rais Samia .
Aidha Rais Samia ameipongeza Wilaya ya Namtumbo kuwa miongoni mwa wilaya zinazozalisha kwa wingi mazao ya biashara ikiwemo,mahindi,Maharage pamoja na
Kahawa inayoongoza kuliingizia Taifa
fedha za kigeni ambazo zinatumika kuleta maendeleo ya nchi.
Katika hatua nyingine Rais Samia akiwa katika
kata ya Rwinga Wilayani humo amesema serikali ipo tayari kuwapa wanachi mbegu
bora za mazao ili kuongeza uzalishaji ,na kusema kuwa serikali itaanza
kuzalisha mbegu, ili kusaidia wakulima kufanya kilimo cha kisasa ili kupata utoshelevu na ziada ya chakula nchini.
Rais wa
Jamuhuri ya muungano wa Tanzania yuko
mkoani Ruvuma kwa Ziara ya kikazi
ya siku 5,Ziara Hiyo imeanzia Wilaya ya Songea ,Ikifuatiwa na Wilaya ya
Nyasa ,na leo yupo Wilayani Namtumbo akiendelea na ziara yake wilayani Tunduru ambapo
ziara hiyo inatarajiwa kuhitimika
septemba 28 mwaka huu.
Mwandishi: Shukuruimana Revocatus
Mhariri: Harieth Kamugisha
0 Comments