Amesema hayo septemba 18,2024 katika
mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam na kusema kuwa maandalizi
ya kuelekea mchezo huo ni ya kiutofauti kulingana na mpinzani wanaye kwenda
kukutana naye septemba 22,2024.
“maandalizi ni makubwa kuelekea mechi yetu
(Simba SC) na Al-Ahli kwa sababu mchezo huu ni wa kiutofauti kulingana na
mpinzani wetu lakini pia mchezo huu ni wa hatua ya mtoano na bado haujaisha uko
50 kwa 50 lazima tujiandae ipasavyo” amesema Ahmed Ally
Ahmed ally amewaomba na
kuwataka mashabiki wa timu hiyo kujitokeza kwa wingi katika uwanja wa Benjamin
Mkapa ili kuwapa hamasa wachezaji na benchi la ufundi la timu hiyo kuelekea
mchezo huo.
“Kila mwanasimba tunapaswa kusimama na timu yetu bila kujali ukumbwa wa mashindano niwaombe na niwatake wanasimba
siku ya jumapili twendeni tukajaze uwanja ili tuipe ushindi simba yetu na
tuingie makundi” amesema Ahmed Ally
Mchezo wa awali ulichezwa katika
uwanja wa Tripoli international stadium mjini Tripoli uliopo nchini Libya ambao
ulitamatika kwa suluhu ya bila kufungana ambapo mchezo wa marudiano utashuhudiwa katika uwanja wa Benjamin Mkapa septemba 22,2024.
Mwandishi; Ramadhani Zaidy.
mhariri;Ellukagha Kyusa
0 Comments