Taifa Stars yapindua meza kibabe dhidi ya Guinea.

Timu ya Tanzania, Taifa  Stars imetakata katika Dimba la ugenini la Charles Konan Banny huko nchini Ivory Coast kwa mabao mawili kwa  moja (1-2), dhidi ya  timu ya Taifa ya Guinea katika mchezo  wa kufuzu AFCON  2025 nchini Morocco.

Mchezo huo umechezwa majira ya saa 1 jioni  kwa masaa ya Afrika Mashariki  huku Tanzania akipata mabao hayo mawili baada ya kutanguliwa na wapinzani wao  kupata goli la kwanza kupitia kwa mshambuliaji wa timu ya Guinea, Mohamed Bayo mnamo dakika 57  baadaya kipindi cha kwanza kutamatika bila kufungana.

Feisal Salum kiungo mshambuliaji wa timu ya Taifa Stars na  Azam FC ya Dar es salam aliweka goli la kuswazisha mnamo dakika ya 61 baada ya kupokea pasi kutoka kwa Wazir Junia na kupiga Shoti kali lililozama kimyani na matokeo kusoma 1-1.

Timu ya Tanzania, Taifa Stars ilionyesha juhudi za kushambulia na kulinda isiruhusu  mashambulizi katika goli lake na mbinu za mwali kwa kufanya mabadiliko kadhaa yaliweza kuwanyima uhuru wapinzani kulifikia lango la Taifa Stars  baada ya kumuingiza Himid  Mao Mkami  na kutuliza Dimba la kati

Taifa Stars iliweza kupata bao la kuongoza mnamo dakika ya 88 kupitia kwa kiungo Mkabaji wa Yanga  Afrika ya Dar es Salaam Mudathir Yahaya kwa kumalizia mpira uliopigwa na kiungo mshambuliaji Feisal na kumshinda mlinda mlango wa Timu ya Guinea Ibrahim Kone na kuifanya Stars kuibuka na ushindi huo.

Tanzania, Taifa Stars imefikisha alama4 ikiwa nafasi ya pili katika kundi H huku Congo DR wakiwa nafasi ya kwanza wakiwa na alama 6 baada ya kushinda mnichezo yao yote miwili kati ya Guinea na Ethiopia, Taifa Stars imebakiza michezo miwili  ya nyumbani kati ya Congo na Guinea kwa ajili ya marudio huku michezo ya nje ni  kati ya Ethiopia na Congo ambao wataanzia nyumbani na kumalizia ugenini.

Mwandishi; Sharifat Shinji 

Post a Comment

0 Comments