Telegram kutoa taarifa za wateja wake kwa vyombo vya usalama..

 


Mwanzilishi wa mtandao wa mawasiliano wa Telegram, Pavel Durov, amesema kuanzia sasa mtandao huo utakuwa unashirikiana na vyombo vya usalama kuwapa taarifa kuhusiana na uhalifu wa watumiaji wake.

Durov, ambaye alikamatwa nchini Ufaransa mwezi uliopita kwa tuhuma za kushindwa kuchukuwa hatua dhidi ya wahalifu kwenye mtandao wake, alisema huduma ya kutafuta taarifa ya Telegram imetumika vibaya na watu wanaouza bidhaa haramu.

Kuanzia sasa, Telegram itakuwa inawapa maafisa wa usalama taarifa kama vile nambari ya simu na anwani ya mtandaoni ya wale wanaovunja kanuni za matumizi ya kimtandao.

Durov, mwenye umri wa miaka 39, yuko nje kwa dhamana, lakini haruhusiwi kusafiri nje ya Ufaransa.

pavel durov alikamatwa mnamo aug 24/8/2024  katika uwanja wa ndege wa le Bouget Airport huku  kukamatwa kwake kukihusishwa na kukataa kushirikiana na vyombo vya usalama juu ya masuala ya ulanguzi wa madawa ya kulevya, biashara haramu ya binaadamu na udanganyifu wa mtandaoni.

Mwandishi; Abel Mahenge.
Mhariri; Eunice Jacob.

Post a Comment

0 Comments