TMA yamuibua waziri mkuu tahadhari ya chakula Nchini

 Waziri Mkuu wa Tanzani Kassim Majaliwa.  (Picha: Bunge)

Waziri mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kassim Mjaliwa amewataka wanachi kutunza chakula walichovuna msimu wa kilimo uliopita kwa uangalifu  hasa katika ngazi ya familia na kuzingatia kanuni bora za uhifadhi wa mazao ya chakula ili kuwepo na usalama wa chakula nchini.

Waziri mkuu ameyasema hayo Septemba 6,2024 wakati akitoa hotuba ya akuhahirisha mkutano wa 16 wa Bunge la Jamhuri ya Muuangano wa Tanzania Jijini Dodoma, na kusisitiza wananchi kutunza chakula ili kuepukana na janga la njaa linaloweza kusababishwa na mabadiliko ya Tabianchi kama ilivyoelekezwa na mamlaka ya hali ya hewa  Tanzania(TMA).

"Nitowe rai kwa wananchi kutumia vizuri mavuno yaliyopatikana  msimu wa  2023/2024 kwa kutunza chakula cha kutosha katika ngazi ya kaya  na  kuzigatia kanuani bora za uhifadhi wa mazao ya chakula" Ameseama Majaliwa.

Akiendelea kutoa rai hiyo Majaliwa amesema baadhi ya mikoa , wananchi wantakiwa kuchukua tahadhari mapema na kuzalisha mazao yanayokomaa kwa muda mfupi zaidi ili kuepuka upungufu wachakula.

"Nachukua nafasi hii kuwahimiza wananchi kupanda aina ya mazao yanayokoma kwa muda mfupi na kustahimili ukame ili kuepuka upungufu wa chakula "

Aidha Mh. Majaliwa amewataka Maofisa Ugani kuhakikisha wanawaelimisha wananchi kuhusu mazao yanayopaswa kupandwa maeneo  yao.


    Moja ya Ghala la hifadhi ya chakula nchini. (Picha na wizara ya Kilimo)

Akizungumza kuhusu uhifadhi wa chakula nchini ameseama serikali kupitia wakala wa uhifadhi wa chakula inaendelea kununua ziada ya mazao ya chakula yaliyopatikana kutoka kwa wakulima kwa ajili ya akiba ya chakula na sehemu ya hifadhi hiyo itatumika kusadia maeneo yatakayobainika kuwa na upungfu wa chakula.

Wakati huo huo Majaliwa ameagiza wizara ya kilimo isimamie kwa karibu upatikanaji wa pembejeo za kilimo hususani mbolea ikiwa ni maandalizi ya  msimu ujao wa kilimo kwa kuzingatia Jiografia za kanda za kilimo nchini.

Mkutano wa 16 wa   Bunge la Jamhuri ya Muungano Tanzania umeputisha Miswada nane ukiwemo mswada wa sheria ya marekebisho ya sheria za hifadhi ya jamii ya mwaka 2024, mkutano huo umehairishwa  hadi Octoba 29,2024.

Mamlaka ya hali ya hewa nchini (TMA) ilitoa tahadhari ya upungufu wa mvua za vuli katika mikoa mbalimbali nchini, Agosti 22, 2024  wakati wakitoa mwelekeo wa msimu wa mvua vuli kuanzia Octoba  mpaka Disemba mwaka huu

Mwandishi; Harieth Kamugisha

 

Post a Comment

0 Comments