1.29 Bilioni kulipa fidia zaidi ya wakazi 724 Kigoma

 


   Waziri wa ujenzi Mh.Innocent Bashungwa


Waziri wa ujenzi Mh. Innoacent Bashungwa amesema  serikali inatarajia kutoa shilling 1.29 billion zitakazo tumika kulipa fidia kwa wakazi zaidi ya 724 ili kupisha ujenzi wa barabara kutoka Kibondo hadi Mabamba mkoani Kigoma. 

Mh.Bashungwa amesema hayo leo bungeni  jijini Dodoma katika kikao cha 16 mkutano wa 5  wakati akijibu  swali la mbunge wa Jimbo la Muhambwe  mkoani Kigoma Dkt Florence Samizi  aliyetaka kujua ni lini serikali italipa fidia ya wananchi wa Muhambwe waliopisha ujenzi wa barabara ya Kibondo hadi Mabamba mkoani humo . 

Aidha waziri Bashungwa ameongeza kuwa serikali imekamilisha tathimini ya mali za wananchi  zitakazoathiriwa na mradi wa ujenzi wa barabara ya Kibondo hadi  Mabamba yenye urefu wa kilometa 47.92 huku   kusisitiza kuwa serikali inakamilisha taratibu zote za malipo ya fidia kwa wananchi hao . 

Mkataba wa ujenzi wa barabara hiyo ulitiwa saini  tarehe 8  Januari 2023 kati ya serikali na kampuni ya ujenzi kutoka  China (CHICO) huku  kazi ya ujenzi wa barabara hiyo ukitarajiwa  kufanyika ndani ya miezi 24  na mradi huo  utagharimu  zaidi ya  shilingi bilioni 63. 


Na mwandishi
:Ramadhani Zaidy

Post a Comment

0 Comments