Wafanyabiashara wa samaki Kasulu wafurahishwa na bei ya samaki.

Wafanyabiashara wa samaki katika soko la  Mnadani,Kata ya Kigondo ,Halmashauri ya mji wa Kasulu , wameeleza kuridhishwa na  bie ya samaki kuendelea kupungua baada ya ziwa Tanganyika kufunguliwa mwezi mmoja uliopita .

Wakizungumza na Buha News bila kutaja majina yao wafanyabiashara hao wamesema kwa sasa bei ya ndoo moja ya samaki aina ya Migebuka  ni shilingi 135,000 Kutoka 165,000 iliyokuwepo wiki moja iliyopita.

“Kwasasasa bei imeshuka tunashukuru sana wiki moja iliyopita tulikuwa tunanunua  165,000/=  ndoo lakini wanaendelea kushuka bei hadi imefikia kiasi cha shilingi 135,000/=  “Alisema mmoja wa wafanyabiashara hao

Aidha Wamesema fungu moja lenye samaki saba hadi nane  linauzwa  shilingi 2000/= kwasasa ambapo awali walikuwa wanauza fungu lenye samaki wanne kwa bei  hiyo  huku akibainisha kuwa ongezeko la wateja limewafanya kuongeza kipato na kukuza uchumikatika familia zao na nchi kwa ujumla.

Ziwa Tanganyika lilifunguliwa  baada ya kufungwa kwa miezi mitatu kuanzia tarehe 15 mei mpaka tarehe 16 agosti mwaka 2024 ,na  baada ya kufunguli kwa ziwa hilo wavuvi na walanguzi wa samaki wanakiri kuona matokeo chanya ya kufungwa kwa ziwa hilo.

Mwaka 2023 kulikuwa na ukosefu wa dagaa na samaki kabla ya ziwa kufungwa, huku  upatikanaji wa samaki na dagaa ukiripotiwa kupande  bei   kufikia  elfu 55  hadi  elfu 60  kwa kilo moja kutoka  elfu 10 ya mwanzo.

Hata hivyo waziri mwenye dhamana Abdallah Ulega wakati akizungumza na wananchi alisema  kufungwa kwa ziwa hilo ni makubaliano yaliyoazimiwa katika kikao kilichofanyika mwaka 2022, kilichohusisha nchi zinazo zunguka ziwa hilo ambazo ni Zambia,Tanzania ,Burundi na Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo  (DRC).

Ifahamika kuwa tarehe 15 mwezi mei mwaka 2024 Ziwa Tanganyika Mkoani Kigoma lilifungwa ili kupisha mazaliya ya samaki pamoja na kukomesha uvuvi haramu,jambo liloleta  taharuki kwa wavuvi wa mikoa inayozunguka ziwa hilo ikiwemo mkoa wa  Kigoma ,Katavi na Rukwa.

Mwandishi; Harieth Dominick.

Mhariri; Eunice Jacob.


Post a Comment

0 Comments