Wakazi wa mtaa wa Mkombozi kata ya
Murusi Halmashauri ya mji Kasulu, mkoani Kigoma wameishukuru Serikali pamoja na Taasisi ya Hope of the community
Foundation kwa kuwaboreshea miundombinu
ya chemichemi ya maji katika mtaa wao.
Wakizungumza na Buha News Septemba 26,2024 baadhi ya wanufaika wa mradi
huo akiwemo Ester Ibrahim, wamesema wamekuwa na changamoto ya hupatikanaji wa maji kwa muda
mrefu kutokana na chanzo cha maji kilichokuwepo
awali kutumika kwa shuguli zote
za mifugo na wanadamu.
"Miaka ya nyuma maji haya
yalikuwa yanatoka machafu sana na pia tulikuwa tunachangia pamoja na mifugo, lakini
pia watu walikuwa wanafua kwenye chanzo hicho , lakini kwa sasa baada ya
kujengewa chemichemi tunafaidika kwa kutumia maji safi na salama ambayo
yanatupa uhakika wa afya zetu kuwa salama"alisema Ester Ibrahim mnufaika
wa mradi.
Nae mkurugenzi wa Taasisi ya Hope
of the Community Foundation Bi.Eveline
Leonard Kahembe amesema taasisi hiyo
ilibaini changamoto ya maji katika eneo
hilo,hivyo kuchukua hatua ya kutatua changamoto hiyo kwalengo la kuwa epusha wakazi
wa eneo hilo na magonjwa ya mlipuko ambayo husababishwa na uchafuzi wa maji katika vyanzo vya maji.
"Tumetembelea chemichemi 5
ndani ya wilaya ya Kasulu Mji tukabaini
uwepo wa changamoto hiyo na adha wanayo pitia wakazi wa maeneo haya tukaona ni
vyema sisi kama taasisi kurudisha faida kwa wananchi kwa kuwaboreshea
miundombinu ya chemichemi hizo"alisema Eveline.
Chanzo cha maji kilichoboreshwa katika kata ya Mkombozi
Nae Afisa mazingira wilaya ya
Kasulu mji Bw.Msafiri Charles ameshukuru uboreshaji wa chemichemi hiyo, na kuwaomba
wadau zaidi kujitokeza kuungana na jitihada za serikali katika kuhakikisha wakazi
wa mji wa Kasulu wanapata maji safi na salama.
Aidha Bw. Msafiri amesema serikali
na wadau wamekuwa wakipeleka miradi ya maendeleo katika jamii hivyo
amewaomba wananchi kuhakikisha wanatunza
miradi hiyo ikiwemo chanzo hicho cha maji ili waendelee kupata maji safi na
salama.
Mpaka sasa Halmashauri ya mji Kasulu kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo na mazingira wameboresha chemichemi tano katika maeneo tofauti ikiwemo Mudyanda, Sunzu, Kanazi, Murusi na Msambala .
Mwandishi: Ellukaga Kyusa
Mhariri:Harieth Dominick
0 Comments