Wakazi wa Kibondo watakiwa kujitokeza kupiga kura na kugombea uongozi serikali za mitaa

 


Wananchi wilayani Kibondo mkoani Kigoma wametakiwa kujitokeza kwa wingi  kujiandikisha na  kupiga kura katika uchaguzi wa serikali za mitaa utakaofanyika kote Nchini mwishoni mwa mwezi Novemba  mwaka huu,ili  kuwachagua viongozi watakaowaletea maendeleo katika maeneo yao.

Rai hiyo imetolewa na Msimamizi mkuu wa Uchaguzi  Halmashauri ya Wilaya ya Kibondo

Deoclets  Rutema  wakati wa mkutano wa kuhamasisha upigaji kura na kutoa elimu

 uliofanyika katika Kijiji cha Kigina kata ya Rugongwe.


 Bw. Rutema amesema ili kuwapata  viongozi bora, katika uchaguzi huo wananchi

 wanapaswa kujitokeza kwa wingi kugombea nafasi za uongozi pamoja na kushiriki

 kikamilifu kupiga kura kuchagua viongozi  sahihi  watakao leta mabadiliko ya  maendeleo

 katika maeneo husika. 

Msimamizi mkuu wa Uchaguzi Halmashauri ya Wilaya ya Kibondo  Deoclets  Rutema  katikati akihamasisha wananchi kujitokeza  kujiandikisha na kupiga kura katika uchaguzi wa Serikali za mitaa

 kujiandikisha katika daftari la kudumu la mpiga kura havihusiki na uchaguzi wa serikali zaMitaa hivyo  wajitokeze kujiandikisha katika daftari la uchaguzi wa  serikali za mitaautakaonza hivi karibuni  .

Bw. Ndarangavye amongeza kuwa kupata viongozi bora  wananchi waepuke kuchagua

 wagombea wanaotoa rushwa ambao hutaka madarada ili kujinufaisha kwa faida yao.

 

Uchaguzi wa serikali za mitaa unatarajiwa kufanyika Novemba 27 mwaka huu,,huku

 uandikishaji wa wapiga kura wa serikali za mitaa ukianza   tarehe 11

 hadi 20 mwezi Octoba 2024  katika mitaa husika na kampeni  za uchaguzi wa serikali za

 mitaa zitaanzaNovemba 20 hadi 26 mwaka huu .


Mwandishi : James Jovin

Mhariri : Harieth Kamugisha 


Post a Comment

0 Comments