Wanafunzi wa darasa la saba kuanza mtihani leo.


                   Wanafunzi wa darasa la saba wakifanya mtihani .

Zaidi ya wanafunzi milioni moja na laki mbili  wameanza mtihani wao wa  kuhitimu elimu ya msingi unaonza leo septemba 11 hadi septemba 12 ,2024   .

Kwa mujibu wa Baraza la mithani Tanzania NECTA watahiniwa wa jinsia ya kike ni laki 6 elfu sitini na sita mia sita na nne (666,604)  ambayo ni sawa na asilimia 54 wakati  wavulana   ni laki tano elfu sitini na nne mia moja  sabini sita  (564,176)  sawa na asilimia 46 ya wavulana wote .

Hata hivyo katika taarifa iliyotolewa  na baraza la mitihani Tanzania septemba 10, 2024  imesema wanafunzi wenye mahitaji maalumu wanaofanya mtihani wa darasa la saba 2024  ni 4583  .

"Wanafunzi wasioona ni 98 ,wenye uono afifu 1402 ,wenye uziwi ni wanafunzi 1067 ,wanafunzi 486 wana ulemavu wa akili pamoja na wanafunzi 1530 wenye ulemavu  wa viungo " Alisema katibu wa baraza la Mitihani Tanzania Dkt  Mohamed

 wakati watahiniwa wa mwaka    2024 wakiwa  1230780  kuna upungufu wa watahini  125,612  ikilinganishwa na watahiniwa  1,397,293 waliosajiliwa kufanya Mtihani wa Kumaliza Elimu ya Msingi mwaka 2023.

Lengo la mtihani  wa kuhitimu elimu ya msingi nikupima maarifa na umahiri waliopata wanafunzi kwa miaka saba na matokeo  yake hutumika kuchagua  wanafunzi watakao jiunga na elimu ya sekondari.


Mwandishi; Ramadhani Zaidy

Post a Comment

0 Comments