Wapalestina takribai 40 wauwawa kusini mwa Gaza

        Picha na BBC

Mkurugenzi wa oparesheni ya mamlaka ya ulinzi na usalama  wa Hamas, amesema kuwa takriban watu 40 wameuawa kusini mwa Gaza na wengine 60 kujeruhiwa katika shambulizi lililofanywa na Israel kwenye aneo lililochaguliwa kuwa la kibinaadamu.

Kwa mujibu wa shirika la utangazaji la BBC Mkurugenzi huyo amesema shambulio hilo limetokea usiku wa kumakia September 10,2024 katika eneo la kibinaadamu la Al-Mawasi magharibi mwa jiji la khan younis.

Kwa upande wa jeshi la Israel kupitia kwa msemaji wa jeshi hilo (IDF) limekiri kuhusika na shambulizi hilo na kusema kuwa ndege yake ilishambulia katika meneo ya khan younis eneo la wapiganaji wa Hamas  na kudai kuwa  ilichukua hatua za kiusalama ili  kupunguza hatari ya kudhuru raia.

 wakazi wa eneo hilo pamopja na mashuhuda wa mlipuko uliotokea  wanasema mlipuko ulitikisa maeneo ya al-Mawasi muda mfupi baada ya saa sita usiku ,na miali ya moto ilionekana kupanda angani  usiku wa shambulizi hilo.

Huu ni muendelezo wa mashambulizi ya jeshi  la Israel (IDF) dhidi ya kikosi cha Hamas kwani  katika juma lililopita wizara ya afya ya Palestina  ilitoa taarifa juu ya kuuawa kwa wapalestina takribani 36 kutoka katika miji ya Jenin na Tubas huku wengi wao wakiwa ni watoto.

Mgogoro huu  wa Israel na Hamas ukanda wa Gaza ulianza octoba 7,2023  baada ya kundi  la  wanamgambo wa Hamas kuishambulia Isreal kwa makombora . 

Mwandishi: Shukuruimana Revokatus.

 

Post a Comment

0 Comments