Watoto milioni 2.8 waathiriwa kielimu na mizozo ya kivita Afrika.

DW

Watoto takribani milioni 2.8 ,Afrika Magharibi  na  Afrika ya kati wameshindwa kuendelea na masomo kutokana na mizozo ya kisiasa katika baadhi ya mataifa katika ukanda huo.

Kutokana na Takwimu zilizotolewa na Umoja wa Mataifa zinaonesha zaidi ya shule 14,000 kutoka nchi 24 zilizopo ukanda wa Sahara na Kongo zililazimika kufungwa katika robo ya pili mwaka huu.

Takwimu hizo  za Umoja wa Mataifa zimebainisha kuwa, shule 1,457 zililazimika kufungwa tangu mwanzoni mwa mwaka mwaka huu , ikiwa Jumla ya watoto milioni 57 wenye umri kati ya miaka mitano hadi kumi na minne kutoka  Magharibi na Afrika ya kati hawahudhurii masomo kutokana na mizozo inayoendelea.

Katika maadhimisho ya siku ya kimataifa ya kulinda elimu, Baraza la wakimbizi la Norway (NRC)  lilisema mataifa yaliyoathiriwa zaidi ni pamoja na Burkina Faso, Mali, Cameroon na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kutokana na mizozo ya kivita inayoendelea .

Mwandishi; Sharifat Shinji

Post a Comment

0 Comments