Israel Yatamba kulipa kisasi Kwa Iran

  Picha na DW

Waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu amesema kuwa nchi yake imepanga kulipa Kisasai   Iran, kutokana na mashambulizi yaliyofanywa na  nchi hiyo mwanzoni mwa juma hili.

Netanyahu amesema hayo Octoba 2,2024 nchini Israel na kusema kuwa kinachofanywa na iran kuishambulia Israel ni kitendo kikubwa cha uchokozi na iwapo Iran haitozuiliwa basi wimbi jengine la makombora halitoilenga tu Israel bali mataifa mengine pia.

Kwa upande wa Rais wa Iran Masoud Pezeshkian ameionya na kutishia kuwa Iran itajibu vikali zaidi, iwapo Israel itathubutu kufanya mashambulizi ya kulipiza kisasi cha mashambulizi hayo.

Naye Rais wa Marekani Joe Biden ambae ndiye mshirika mkubwa wa Israel siku ya  Jumatano alisema kuwa hatoiunga mkono Israel iwapo itashambulia miundombinu ya zana za nyuklia za Iran.

Iran ndiye mdhamini mkuu wa makundi ya Hamas Pamoja na Hezbollah Ambayo ni  msingi wa  mgogoro huo, huku Umoja wa Mataifa ukiripoti kuwa Iran imetuma  makombora karibu 200 Israel ili  kuizuia Israel kutoendelea na mashambulizi yake  .

Mwandishi :Ramadhani Zaidy

Mhariri: Harieth Kamugisha 

Post a Comment

0 Comments