
Buha News imemtafuta Ofisa Kilimo wa Halmashauri ya
mji wa Kasulu Zephania Sodya kufahamu ikiwa tayari utekelezaji wa agizo
hilo umeanza mjni hapa .
Akizungumza na Buha News, Bw. Zephania Sodya
amesema kwa kushirikiana na
shirika la World Vision kupitia Mradi wa Kilimo Tija Kigoma (KITIKI) wenye
lengo la kuhamasisha kilimo cha mazao ya Mahindi,Alizeti na Maharage wameendelea kutoa elimu kwa wakulima kuanzia
upandaji wa Mbegu hadi kuvuna mazao kwa kata zote.
“Tunawafikishia wakulima elimu hiyo hata kabla ya
agizo la waziri mkuu ,elimu ya namna ya kupata mbolea ya ruzuku,aina ya
mbegu za kupanda kulingana na eneo husika na tunafuatilia
maelekezo ya mamlaka ya hali ya hewa ili tuweze kuwasaidia wakulima na hatuna
shaka wakulima wanaelimu ya kutosha kwasababu tuna wakulima viongozi
wanaoongoza vikundi vya wakulima katika kata zote” anasema Bw. Sodya.
Afisa kilimo pia amesema upatikanaji wa mbolea ya ruzuku ni toshelevu kwa mji wa Kasulu hivyo amewashauri wakulima wasiyo na namba kujisajili mapema ili wapate Namba itakayowawezesha kupata mbolea ya Ruzuku na kusisitiza wakulima waliosajiliwa mwaka jana watatumia namba zao za awali .
Wakizungumza na Buha News ,kwa njia simu wakulima kutoka kata tofauti akiwemo Dorothea Ntibinona kutoka kata ya Mhunga kijiji cha Marumba amekiri kupata elimu ya kilimo chenye tija na kwamba elimu inaendelea kutolewa kuhusiana na matumizi ya mbegu bora , ,mbolea na viwatiliu ingawa changamoto kubwa walionayo ni ukosefu wa masoko ya mazao yao.
Bi Dorothea ameongeza kuwa changamoto nyingine ni ukosefu wa pembejeo za Ruzuku katika maeneo yao ,hivyo hulazimika kusafiri kwa gharama za ziada kufuata Pembejeo
mjini hali inayoongeza usumbufu na
kupoteza muda wa kufanya shughuli nyingine za kimaendeleo .
“Nauli ya kutoka hapa kijijini ni 4000 kwenda na
kurudi 8000 bado ujalipa ghrama ya kubeba
Mbolea kutoka Kusulu hiyo gharama kubwa kwa mkulima kumbuka mazao tunapata, ila hatuna soko la kuuza kwahiyo hizo ndiyo
changamoto zetu “Alisema Dorothea .
Nae mkulima
kutoka kata ya Nyachenda ambaye hakupenda
jina lake litajwe amekiri kufikiwa na elimu ya kilimo bora ambayo imeleta
mbadiliko chanya kwa wakulima,na uzalishaji
wa mazao umeongezeka lakini anataja changamoto ya soko kuwa kizungumkuti
hali inayoendelea kusababisha umaskini kwa wakulima.
“Mwanzo
nilikuwa nalima robo heka napata debe nne au tatu pekee lakini baada ya kupata elimu ya
kilimo bora ,nikaanza kulima zao moja mwanzo tulikuwa tunachanganya mazoa
,nikaanza kufua na sentimita za kupishana kati ya mbegu moja na nyingine nazingatia
pia aina za mbegu kulingana na hali ilivyo ,nafuata pia utaratibu wa uwekaji
mbolea na kwasasa navuna hadi gunia 4 hadi 5 kwa robo heka, lakini hakuna soko la
kuuzia” Alisema mkulima huyo.
Kwa upande wake Kiongozi wa wakulima kutoka kijiji cha Marumba
Kata Muhunga anayeongoza vikundi zaidi ya sita vya wakulima katika eneo hilo Asela Richard Lulangara amesema elimu
imewafiki na wameongeza uzalisha lakini
bado kuna changamoto ya ukosefu wa soko pamoja na upatikanji wa mbolea katika
maeneo yao ,ambapo wameitatua chanamoto
hiyo ya kukosa mbolea kwa kushirikiana
na shirika la World Vision Kigoma kupitia Mradi wa Kilimo Tija Kigoma (KITIKI) wanawasaidia wakulima kupata mdau anayeleta mbolea katika maeneo
yao.
“Tunakusanya Hela zetu kupitia kuweka hisa kisha kila mkulima ananunua mbolea kulingana na uhitaji wake alafu World Vision wanatutafutia mdau anayeleta mbolea kijijini kulinga na mahtaji ya wakulima ” alisema Bi.Asela .
Katika hatua nyingine Bi. Amina Yusuph mkulima kutoka Kata Kidyama
amesema yeye hajabahatika kupata elimu ya Kilimo bora na anaendelea kulima
kilimo cha za zamani .
“Mimi sijawai kuwaona maafisa kilimo labda wakipita huku huwa nakuwa nyumbani au kwenye biashara zangu
nyingine” alisema Bi Amina.
Akizungumzia changamoto ya ukosefu wa Soko la mazao Ofisa
Kilimo Halmashauri ya mji Kasulu Bw. Zephania Sodya amekiri kuwepo kwa changamoto hiyo kwa
wakulima na kubainisha kuwa wanaendelea kukabiliana na changamoto hiyo kwa kushirikiana
na maofisa ushirika kuanzisha vyama vya
Ushirika ambavyo vitasaidia upatikanaji wa soko kwa wakulima.
“Tayari tumeanzisha AMCOSS kata ya Mwilamvya,Kijiji cha
Ruhita,kijiji cha Karuta ,Mwanuhe kata ya Heru juu na Kata Msambara Lengo ni
kuwawezesha wakulima kupata masoko ya kuuza mazo yao kupitia vyama vyao vya
ushirika na tunatarajia ndani ya miaka 3 ijayo wakulima wataanza kuona matokeo
chanya ya vyama hivi ” Alisema Afisa Kilimo.
Kuhusu upatikanaji wa Mbolea ya Ruzuku Ofisa kilimo
huyo amesema wako baadhi ya mawakala wanaopeleka mbolea vijijini lengo ikiwa
nikuwasaidia wananchi wapate mbolea hizo maeneo yao.
Mamlaka ya hali ya hewa Tanzania (TMA) ilitoa utabiri wa hali ya hewa Mwezi Agusti mwaka huu ,wakati wakitoa
mwelekeo wa mvua kuanzia Mwezi Octoba
hadi Desemba 2024 ulionesha uwepo wa upungufu wa mvua za msimu wa
vuli,utabiri uliomfanya waziri mkuu wa Jamuhuri wa Muungano wa Tanzania Kasimu
Majaliwa kutoa maelekezo kwa maafisa
ugani nchi nzima ili kuepuka upungufu wa
chakula unaoweza kujitokeza kwa kutokuchua tahadhari ya mapema .
Mwandishi:Harieth Kamugisha
Mhariri: Sharifat Shinji
0 Comments