Watu zaidi ya 70 wahisiwa kufariki DRC baada ya Feri Kuzama ziwa Kivu

 

Takribani watu 78 wanahisiwa  wamefariki dunia na wengine kunusurika kifo baada ya feri kupinduka  na kuzama katika Ziwa Kivu, mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

Taarifa zinasema kuwa meli hiyo iliyokuwa imewabeba abiria zaidi ya 278  na mizigo, ilizama muda mfupi kabla ya kuwasili katika bandari ya mjini Goma ikiwa inatoka kwenye mji wa Minova katika jimbo jirani la kivu kusini .

 Kulingana na vyanzo vya ndani , meli hiyo kwa jina la Merdy, ilipinduka  saa nne asubuhi Octoba 3,2024  kwenye ziwa Kivu katika eneo la umbali wa karibu meta 200 hadi kwenye soko kuu la kituku .

 Watu wachache walionusurika wamefikishwa mjini Goma wakiwa katika hali mahututi na wengine walifariki muda mchache  baada ya kufikishwa Hosptali wakiwemo watoto wawili.

 Nae gavana wa jimbo la Kivu kusini Jean Jacques Purusi amesema  Kulikuwa na abiria 278 ndani ya boti hiyo , 

Kwa mujibu wa BBC  gavana wa mkoa huo amesema   itachukua angalau siku tatu kupata idadi kamili, kwa sababu bado miili  yote haijapatikana.


Mbali na abiria waliokuwemo, meli hiyo pia ilikuwa imebeba shehena ya chakula na vifaa vingine muhimu kutoka katika mji mdogo wa Minova jimboni kivu kusini.  

 Ziwa kivu, ndilo limesalia kuwa njia pekee inayotumiwa kusafirisha bidhaa kwenda katika mji wa Goma, tangu kufungwa kwa barabara na wapiganaji wa kundi la M23 miezi michache iliyopita

Ajali hiyo imetokea ikiwa ni Miaka miwili iliyopita tangu , watu wasiopungua 55 kufariki dunia baada ya  boti iliyojaza abiria kuliko uwezo wake ilipozama kwenye mto kongo katika jimbo la mongala kaskazini mwa DRC .

Mwandishi: Ellukaga Kyusa 

Mhariri: Harieth Kamugisha.

 

Post a Comment

0 Comments