Rais Dr Samia ataka Amani kuendelea kudumishwa zoezi la upigaji kura


Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dr Samia Suluhu Hasan ametaka Amani na utulivu kuendelea kudumishwa katika kipindi chote cha zoezi la upigaji kura wa serikali za mitaa.

 Rais Samia amesema hayo baadaya kupiga kura katika kijiji cha Chamwino,Jijini Dodoma ambapo amesema zoezi la upigaji kura ni utamaduni wa kawaida wa kidemokrasia hivyo hakuna sababu za mivurugano na matokea yatolewe kama yatakavyoamuliwa na

wananchi.

 Uchaguzi wa serikali za mitaa unahusisha jumla ya Vijiji 12,333, Mitaa 4,269 na Vitongoji 64,274 nchi nzima.

Mwandishi: Harieth Dominick .

 


Post a Comment

0 Comments