Rais Samia atuma salamu za pole kufuatia kifo cha Dr Ndungulile

 



Rais Samia Suluhu Hassan ametuma salamu za pole  kwa familia na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzaniaza kutokana na  kifo cha Dk Faustine Ndugulile, Mbunge wa Kigamboni na Mkurugenzi Mteule wa Shirika la Afya Duniani

(WHO), Kanda ya Afrika.

“Nimepokea kwa masikitiko taarifa ya kifo cha Dk Faustine

Ndugulile, Mbunge wa Kigamboni na Mkurugenzi Mteule wa

Shirika la Afya Duniani (WHO), Kanda ya Afrika, kilichotokea

usiku wa kuamkia leo Novemba 27, 2024.”


“Ninatoa salamu za pole kwa familia, Spika wa Bunge la

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dk Tulia

Ackson, wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa

Tanzania, wananchi wa Kigamboni, ndugu, jamaa, marafiki

na Watanzania wote.” Ameandika Rais Samia.


Dk Ndugulile alikuwa Mkurugenzi mteule wa Shirika la Afya

Dunia Kanda ya Afrika (WHO) ambaye alipaswa kuanza

majukumu hayo mapya Februari 2025.

Mwandishi:Harieth Dominick .

Post a Comment

0 Comments