Walioomba ajira Kigoma wamshangaza Naibu waziri

 

Mkoa wa kigoma umetajwa kuwa ni miongoni mwa mikoa yenye idadi ndogo ya watu walioomba ajira katika kada ya Afya.

Naibu waziri Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Deus Sangu leo ameonesha kushangazwa na jambo hilo huku akitaja sababu kuwa ni kukwepa maeneo ya vijijini.

Amesema hatua hiyo ni matokeo ya Sekretarieti ya ajira katika utumishi wa umma kuweka utaratibu wa kuomba ajira katika mikoa husika kulingana na uhitaji.

Sekretarieti ya ajira kwa mwaka huu mwezi Juni ilitangaza nafasi za kazi 9,483 katika kada ya Afya ambapo kila muombaji alilazimika kuomba ajira katika mkoa ambao atafanya kazi.

 “Vijana wengi wanaomba ajira huku wakiwa na malengo ya kufanya kazi katika majiji makubwa jambo ambalo kiuhalisia ni gumu” alisema Mhe.Sangu.

Mhe. Sangu ametoa mfano katika Mkoa wa Kigoma kuwa watumishi kada ya Afya wanaohitajika ni 400 lakini maombi yaliyopokelewa ni 200 pekee.

Mikoa ya Lindi, Mtwara na Katavi nayo ni miongoni mwa mikoa yenye idadi ndogo ya maombi ya ajira katika kada hiyo, ukilinganisha na uhitaji wakati Mikoa ya Dar es salaam, Mwanza na Dodoma ikiwa na idadi kubwa ya waombaji.

Mwandishi: Mussa Mkilanya

Post a Comment

0 Comments