Mume/Mke washikiliwa na jeshi la polisi Mbeya kwa tuhuma za kukatisha maisha ya mtoto wao

 

JESHI la Polisi Mkoa wa Mbeya linawashikilia watuhumiwa wawili ambao ni Ramadhan Tembo Mwakilasa (28) na Mariamu Charles Mwashambwa (28) Wakazi wa Jiji la  Mbeya kwa tuhuma za mauaji ya mtoto Chloy Ramadhan [04] kwa kumpiga fimbo sehemu mbalimbali za mwili.

 Tukio hilo limetokea Novemba 25, 2024 saa 2:00 usiku Mtaa wa TEKU viwandani , ambapo mtoto huyo alifariki dunia baada ya kupigwa fimbo sehemu mbalimbali za mwili wake na baba yake mzazi  Ramadhan  Mwakilasa  akishirikiana na mama yake wa kambo aitwaye Mariamu Charles Mwashambwa (28).

Uchunguzi umebaini kuwa chanzo cha tukio hilo ni ukatili na unyanyasaji wa kumuadhibu mtoto huyo  baada ya kujisaidia kwenye nguo alizokuwa amezivaa.

 Jeshi la Polisi limewataka wazazi/walezi kuacha vitendo vya ukatili kwa watoto vinavyokatisha  maisha yao kwa kisingizio cha makosa  badala  yake watumie njia sahihi za kurekebisha  zisizo na madhara kwa watoto.

Mwandishi:Harieth Doinick 

Post a Comment

0 Comments