Acheni mirathi mapema kuepusha mifarakano ya familia - Kimilomilo.

 

Wakili wakujitegemea Hamis Ramadhani Kimilomilo amewaasa wananchi kuepuka tamaa za Mali pale mmiliki anapofikwa na umauti.

 Ameyasema hayo Ofisi kwake wakati akifanya mahojiano na Buha FM radio leo juu ya umuhimu wa kuandika mirathi na kusema kuwa wapo baadhi ya wananchi wanaokiuka mirathi iliyoachwa na mmliki baada kufariki jambo ambalo linakuwa chanzo cha migogoro ndani ya familia 

 "Unapo kiuka na kuingiza tamaa ya Mali inakuwa chanzo cha ugomvi na wengine kujichukulia sheria mkononi kuua au kujeruhi Moja kwa moja unakumbana na adhabu ya makosa ya mauaji au kujeruhi "alisema Wakili Kimilomilo.

 Wakili Kimilomilo amesema upo umuhimu wa kuandaa mirathi kwa wamiliki wa mali kwakuwa inasaidia kuepuka migogoro ya kifamilia.

 "Wananchi ondoeni hizo kasumba kwamba ukiandaa mirathi unajichulia kifo hapana tambua kuwa mali hizo umetafuta kwaajili ya familia unapofariki bila mchanganuo wowote inatengeneza migongano ya kifamilia hasa ukikutana na watoto au ndugu wenye tamaa"Ameongeza Wakili Kimilomilo.

 Godhope Isaya,Erick Erick na Samwel Kajula ambao ni wananchi Kasulu Mji Mkoani Kigoma wamesema kuwa umuhimu upo wa kuandaa mirathi kwasababu inasaidia kupunguza kesi mahakama za mwanzo, Baraza la ardhi na kuepusha mfarakano ndani ya familia.

 "tunashudia kesi nyingi za mirathi katika mabaraza ya ardhi na hata mahakama za mwanzo na chanzo chake nikutokuwa na uwazi wa mali anazo miliki baba au Mama kwenye familia inapotokea kifo migongano na chuki zinaibuka kwenye familia" walisema Wananchi.

 Wananchi hao wameiomba Serikali na mahakama kutoa elimu kupitia vyombo mbalimbali vya habari kuwajengea wananchi uwelewa wa mirathi.

 " Tunaomba Serikali kupitia bunge wasisitize kuhusu sheria ya mirathi lakini mahakama zetu pia watoe elimu kupitia vyombo vya habari kwani tunaamini kuwa wapo wenzetu ambao hawajui, hawajawahi kusikia juu ya umuhimu wa jambo kama hilo" waliongeza wananchi.

 Mahakama ya mwanzo kasulu Mji katika kipindi cha mwaka 2024 zimefunguliwa kesi zaidi ya 60 zinazohusiana na mirathi.


Muandishi : Eunice Jacob.
Mhariri      : Mussa Mkilanya.

Post a Comment

0 Comments