Akizo hilo amelitoa leo wakati akizungumza
na madereva Bajaji katika eneo la stendi mpya wilayani kasulu huku akiwataka
kupata mafunzo ambayo yamekuwa yakitolewa ili wawezekupata vyeti
vitakavyowasaidia kupata Leseni za udereva wa vyombo vyao.
“Ili tuweze Kwenda vizuri kwenye hii
sikukuu lazima tufuate sheria na kanuni za barabarani kwa sababu muda huu
safari zinakuwa zinahitajika kwa kiasi kikubwa sio mizigo sio abiria sasa
haitupi nafasi ambayo itatufanya tuvunje sheria na wale waliofunga viti pembeni kwenye bajaji zao mkavitowe kama huna leseni tafuta leseni fanya kazi yako” Amesema Kamanda Damas.
Aidha kwa upande wake katibu wa waendesha Bajaji Hamis Juma Mkuyu amesema watatekeleza kile kamanda wa usalama barabarani alichowaagiza huku akitaka mafunzo yawe yanatolewa kila wakati ili kuwasaidia Madereva Kubadilika na kupata elimu inayotolewa.
“Naungana na kile alichokisema mkuu wa
usalama barabarani aliyoyazungumza ni sawa kabisa na nimshukuru lakini naomba
elimu hii iendelee kutolewa kila mara kwani madereva ni watu wa kubadilika lakini
nitaendelea kushirikiana na viongozi wenzangu kuhakikisha matukio ya ajari
barabarani yanapungua kwa kufuata sheria za usalama barabarani” Amesema Mkuyu.
Bilali Bakari ambaye ni mwendesha bajaji na
mwenyekiti wa nidhamu katika kijiwe cha Bajaji Mnadani amesema madereva
wanatakiwa kufauata taratibu na sheria zilizowekwa na vijiwe ili kupunguza
matukio na changamoto zinazojitokeza katika vijiwe hivyo.
“Mimi kama mwenyekiti wa nidhamu kijiwe cha bajaji Mnadani nimewambia ni marufuku bajaji inayotoka mjini haitakiwi kupaki
mkono wa kushoto inatakiwa ipaki mkono wa kulia nimeongea nao wote na
wamenisikiliza na abiria anapoona bajaji inawatu watatu wanne asipande kwani
huo ni uvunjifu wa sheria za barabarani” Amesema Bilali.
Jeshi la Polisi kitengo cha usalama barabarani kwa kushirikiana na chuo cha VETA Nyumbigwa limekuwa likitoa mafunzo kwa madereva wa vyombo vya moto hasa Bajaji na Pikipiki ili kupunguza ajari zinazopelekea kupoteza Maisha na ulemavu wa kudumu kwa raia wengi nchini.
0 Comments