Epukeni taarifa potofu mikopo ya Halmashauri inatolewa kwa vikundi

 

Mratibu wa mikopo katika Halmashauri ya mji Kasulu Bwn. Godfrey Jeremiah ambae pia ni Afisa maendeleo Halmashari ya mji Kasulu amewatoa hofu wakazi wa Kasulu kuhusiana na mikopo ya asilimia 10 inayotolewa na Halmashauri.

 Akizungumza na Buha fm katika kipindi cha darasa nje ya shule leo ameeleza kuwa kuwekuwa na taarifa potofu kuwa usajili wa vikundi unafanyika kwa udanganyifu na kwamba tayari wapo watu ambao wamesha andaliwa kupewa mikopo hiyo jambo ambalo sio la kweli.

Ameeleza kuwa mikopo ya Halmashauri bado inatolewa na elimu juu ya mikopo hiyo pia inaendelea kutolewa kwa vikundi mbalimbali kupitia kata husika.

“Ikitokea mtu au kikundi kinahitaji uelewa kuhusu namna ya kuandaa na kusajili kikundi chao wasisite kututafuta kwa maana kila kata ina afisa aendeleo ya jamii ambae miongoni mwa majukumu yetu ni kutoa elimu kwa jamii lakini pia kufatilia maendeleo ya kikundi husika kabla na baada ya kupata mkopo,” amesema Godfrey.

Kauli ya hiyo ni baada ya kuwepo baadhi wa wakazi wa Halmashauri ya mji Kasulu hasa wanawake kuelezea kuhusu ukosekanaji wa elimu juu ya mikopo hiyo na kupelekea kuamini kwamba kufuata taratibu za kusajili vikundi kisheria ni kupoteza muda.

Mikopo ya Halmashauri ni mikopo ambayo ni asilimia 10% ya mapato ya Halmashauri husika na inatolewa kwa makundi

maalumu ya wanawake, vijana pamoja na walemavu kwa kuzingatia muongozo wa kikundi husika.

Mwandishi: Ellukagha Kyusa.

Mhariri      : Mussa Mkilanya.

 


Post a Comment

0 Comments