King Class Sports yadhamiria kukabiliana na Changamoto za mabondia Nchini.


 Bondia wa Ngumi za kulipwa nchini Ibrah class amewaasa mabondi wanaochipukia kuwa wavumilivu katika mchezo wa Ngumi, huku akisisitiza kujituma katika mazoezi na kucheza mchezo kwa uwezo wao.

Hayo ameyasema jana wakati akizindua Kampuni iliyochini yake ya uendeshaji mchezo wa ngumi aliyoipa jina la King Class Sports.

Bondia huyo ameongeza kuwa kampuni hiyo imedhamiria kuibua na kuendeleza vipaji vya mabondia wazawa kwani kampuni yake imejipanga kukabiliana na kuondoa changamoto zote ambazo wanakutana nazo mabondia wengi wa changa hapa nchini.

“Sasa nimepiga hodi katika Upromata, mabondio tumekuwa tukizulumiwa sana katika mchezo huu, wakati mwingine hapewi hata mapambano japokuwa tunajiandaa na kuwa tayari kucheza hivyo unajikuta unatumia muda mrefu kuonesha kipaji chako, hili halitakuwepo King Class Sports,” amesema Ibrah.

Aidha Bondia huyo ameongeza kuwa sikuzote mwanzo ni huwa ni mgumu lakini King Class Sports imejipanga kusaidia vipaji vya ngumi kucheza ndani ya Tanzania na Nje ya Tanzania.

Bondia Ibrah ametambulisha mabondia watatu ambao wameingia mkataba wa makubaliano ya kufanya kazi na kampuni hiyo ambao ni Issa Mollel bondia Mmasai, Rahimu Khalid Omary na Jawabu Habibu Kinyogoli.

Bondia Ibrah Class kwa sasa Tanzania ni Bondia wa pili kwa ubora amecheza mapambano 38 kati ya mapambano hayo ameshinda mapambano 28 na mapambano 15 ameshinda kwa KO.

Mwandishi: Mussa Mkilanya.


Post a Comment

0 Comments