Mwasisi wa Buha FM achaguliwa kuwa mjumbe wa Bodi MISA-Tanzania.

 

Mwasisi na mtendaji mkuu wa kituo cha habari cha Buha FM Radio inayopatikana Mwilamvya, Wilaya ya Kasulu  Mkoani Kigoma Ndg. Prosper Kwigize amechaguliwa kushika nafasi ya ujembe wa Bodi ya uongozi wa Taasisi ya vyombo vya habari kusini mwa Afrika Tawi la Tanzania (MISA-TAN).

Katika uchaguzi huo uliofanyika Novemba 04 mwaka huu jijini Dodoma Ndg. Kwigize amepata kura 31, akifuatiwa na Alex Benson Sichona kutoka chuo kikuu cha Dar es Salaam aliyepata kuwa 28.

Aidha kwa upande wa Mwenyekiti wa Misa-Tanzania Ndg. Edwini Soko ameshinda nafasi hiyo akipokea kijiti kutoka kwa Salome Kitomari ambaye alikuwa mwenyekiti wa taasisi hiyo kwa muda wa miaka nane.

Akitangaza matoke hayo Mwenyekiti wa kamati ya uchaguzi Ali Aboth, ambaye pia ndie msimamizi wa uchaguzi huo akitangaza matokeo hayo, amemtangaza Edwin Soko kuwa Mwenyekiti mpya wa Misa -Tan kwa kupata kura 33, akifuatiwa na Said Mmanga aliyepata kura 9 na nafasi ya tatu ikichukuliwa na Betty Masanja aliyepata kura 3 wakati kura moja ikiharibika.

Katika uchaguzi huo jumla ya wajumbe waliopiga kura walikuwa 46 na viongozi waliochaguliwa wataongoza taasisi hiyo nyeti ya vyombo vya habari na waandishi wa habari kusini mwa Afrika tawi la Tanzania kwa kipindi cha miaka mitatu (3).

MuandishiMussa Mkilanya.


Post a Comment

0 Comments