Mkurugenzi wa Halmashauri Kasulu Mji awataka Viongozi wa mitaa na kata kusimamia usafi Mazingira

 

Katika kuadhimisha miaka 63 ya Uhuru wa Tanganyika leo Halmashauri ya mji Kasulu imetekeleza agizo la Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan la kufanya maadhimisho hayo kwenye maeneo ya kijamii.

 Akizungumzia maadhimisho hayo mkurugenzi wa Halmashari mji Kasulu Mwl. Vumilia Simbeye amesema lengo la kufanya usafi katika Hospitali hiyo ni kuhakikisha mazingira ya hospitali  yanakuwa safi .

 Mwl. Simbeye ameelekeza watendaji wa kata na mitaa kuhakikisha wanafuatilia hali ya usafi wa mazingira katika maeneo yao.

 Kwa upande wake Katibu Tawala wilaya Kasulu Bi,Theresa Mtewele amewasisitiza wananchi kuwa wazalendo kwa kushiriki katika shughuli za kijamii ikiwemo kuimarisha usafi wa mazingira.

 Mkuu wa Jeshi la polisi Wilaya ya Kasulu SSP Sango amesema  jeshi la polisi litaendelea na  zoezi la usafi ili na kuhakikisha vichaka vyote vinavyotumiwa na wahalifu vinafyekwa.

 Aidha SSP Sango amesema suala la usafi ni jukumu la kila mmoja bila kujali siku za   maadhimisho, huku akiwataka wananchi kufichua wahalifu ili kuendelea kudumisha Amani na Utulivu ulioachwa na muhasisi wa taifa Mwl Julius Kambarage Nyerere.

Haya ni maadhimisho ya miaka 63 ya uhuru wa Tanganyika huadhimishwa December 9 ya kila mwaka.

Mwandishi:Ellukaga Kyusa

Mhariri:Harieth Dominick.

Post a Comment

0 Comments