Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu, Dkt. Semistatus Mashimba leo Desemba 9. 2024, ameongoza zoezi usafi katika Hospitali ya Wilaya ya Kasulu na vituo vyote vinavyotoa huduma za afya lililoambatana na uchangiaji wa damu kwa kushirikiana na Kambi ya Jeshi ya 825 Mtabila.
Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi, Afisa Usafi na
Udhibiti wa Taka wa Halmashauri hiyo, Ndelekwa Vanica amehimiza jamii kushiriki
mazoezi ya usafi ya kitaifa likiwemo lile la kila Jumamosi ya mwisho wa mwezi
ili mazingira yawe safi.
“Serikali imeshatoa tamko kila Jumamosi ya mwisho wa
mwezi ni wajibu wa kila mwananchi kushiriki shughuli za usafi, na niwaombe
Kambi ya mtabila kila tutakapowaita katika mazoezi hayo mje kama njia mojawapo
ya kuhamasisha jamii kushiriki usafi huo” amesema.
Naye Kaimu Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya ya
Kasulu Mageni Pondamali ameishukuru Kambi ya JKT Mtabila kwa kuchangia damu
kutokana na hospitali hiyo kuwa na uhaba wa huduma uliokuwepo hospitalini hapo.
Na mwandishi wetu.
0 Comments