Medical Teams International yapongezwa kwa kuhudumia wakimbizi wenye mahitaji maalumu


Unyanyapaa kwa watu wanaoishi na Virusi Vya Ukimwi katika kambi za wakimbizi umetajwa kudumaza jitihada za mapambano dhidi ya UKIMWI na kusababisha msongo wa mawazo kwa watu wanaishai na maambuki.

Hayo yamebainishwa Watu wanaoishi na VVU katika kambi ya wakimbizi ya Nduta wakati wa maadhimisho ya siku ya Ukimwi duniani yaliyofanyika jana katika kambi ya wakimbizi wa Burundi ya Nduta ikiyopo wilayani Kibondo mkoani Kigoma

Mmoja wa watu wanaoishi na virusi vya Ukimwi kwa miaka 13 ambaye hakutaka majina yake yatajwe amebainisha kuwa  wamekuwa wakiitwa majina mabaya yanayokatisha tamaa ya kuishi.

"Wanadiriki kutuita tumeoza ,wafu na maneno mengi ya udharirishaji licha ya kwamba sisi hatuna shida tunajua hali zetu na tunaweza kufanya kila kitu “alisema Mama huyo mwenye watoto 4 wasiyo na maambukizi

Kwa upande Bakuru Ephraim ambaye pia ameishi na VVU Kwa miaka 16 anasema kutokujitambua kwa baadhi ya watu ndiyo chanzo Cha unyanyapaa Kwa watu wanaoishi na VVU.

"Kama unavyoniona huwezi jua kama Nina Virusi vya Ukimwi na anafanya kila kitu na Nina watoto saba wote hawana Ukimwi hata Mke wangu hana maambukizi ya VVU Kwa sababu tunafuata maelekezo ya Wataalam wa Afya " Alisema Bukuru

Bukuru ambaye ni mkimbizi wa Burundi anabainisha kuwa Watu wajue Virusi vya Ukimwi ni kama Magonjwa mengine ya moyo, Kansa,Kisukari ambayo watu wanaishi nayo maisha yao yote wakizingatia maelekezo ya madaktari

“Tunapongeza na kushukuru Mashirika yanayohudumia wakimbizi chini ya UNHCR hususani taasisi ya Timu za Afya ya Kimataifa (Medical Teams International –MTI) kwa namna wanavyotoa huduma mbalimbali za afya kwa wakimbizi na usaidizi wa kiafya na kijamii kwa watu wanaoishi na virusi vya Ukimwi, bila MTI maisha yetu yangekuwa hatarini” Alisisitiza Bw. Bukuru

Katika Maadhimisho hayo ambayo yaliunganishwa pamoja na siku ya Ukimwi duniani ikiratibiwa na shirika la timu za afya kimataifa (MTI) na Baraza la wakimbizi la Denmark (DRC) imebainishwa kuwa watu wenye ulemavu na wanaoishi na virusi vya UKIMWI husahaulika katika vipaumbele vya utoaji wa huduma.

Inaelezwa kuwa jamii ya wakimbizi wenye virusi vya ukimwi na wenye ulemavu wamekuwa wakisahaulika wakati wa utoaji wa huduma za kijamii ikiwemo ulinzi.

 Akisoma risala kwa niaba ya watu wenye ulemavu Bw. Chongera Elias raia wa Burundi anashukuru jumuiya ya kimataifa kupitia UNHCR wanaotoa huduma kwa wakimbizi na kueleza kuwa pamoja na kuwepo kwa changamoto kadhaa Mashirika hayo yanajitoa kuhakikisha jamii ya watu wenye mahitaji maalumu wanapatiwa huduma stahiki.

 Bw. Chongera alibainisha kuwa kuwa licha ya huduma zinazotolewa kwa watu wenye ulemavu na wanaoishi na virusi vya ukimwi, bado kuna ombwe la changamoto kadhaa ambazo Mashirika ya misaada yanapaswa kuzitatua ili kuwarahisishia maisha watu hao.

 Bw. Chongera Elias raia wa Burundi akisoma risala kwa niaba ya watu wenye ulemavu katika maadhimisho hayo Kambi ya Nduta.

“Sisi tunaoishi na ulemavu tunakabiliwa na shida nyingi, licha ya kwamba tunapata misaada wakati mwingine tunahitaji usaidizi Zaidi mfano wakati wa kusafirisha vyakula kutoka kituo cha ugawaji hadi majumbani na hata wakati wa kurejea nyumbani kwa wanaohiyari kufanya hivyo, unajua sisi watu wenye ukemavu inapotokea vita au machafuko yoyote sisi ni wahanga Zaidi na wanapaswa kulindwa hata ukimbizini. Alisisitiza Bw. Chongera mwenye ulemavu wa viungo.

 Nae Dkt .Godlove Kanyonga kutoka Medical team International, kitengo Cha Afya ya akili  na Utengemano anasema kambi ya Nduta kuna maambukizi mengi ya Ukimwi akitaja kuwa katika kiindi cha Januari hadi Decemba mosi mwaka huu MTI ilibaini kuendelea kuwepo na maambukizi mapya na ina jumla ya  watu wapya 37 walibainika kuwa na maambukizi, wanawake 15 na wanaume 12 katika Kambi ya Nduta na wote wanapatiwa matibabu ya dawa na ushauri nasihi .

Kwa upande wake Mratibu wa Elimu Kwa watu wanaoishi na VVU/UKIMWI Kutoka shirika la Medical Team International (TMI) Calen Amos amesema maadhimisho hayo wameyaunganisha na siku ya walemavu duniani ili kuwapaelimu watu wenyelemavu kuhusu maambukizi ya VVU kwa kuwa ni kundi linaloguswa pia na maambukizi ya hayo.

"Tumeamua kushirikiana na mashirika Mengine ikiwemo DRC kuunganisha na siku ya walevu Kwa sababu ni miongoni mwa kundi ambalo halina Elimu na tunataka na wao wapate Elimu maana pia wako watu wenye ulemavu wanaoishi na maambukizi VVU" Amesema Kalen.

Calen amesema katika kampeni za kuelekea siku hiyo walipima watu zaidi ya 700 na wakabaini watu 2 wenye maambukizi, huku jumla ya watu 360 katika Kambi hiyo wanaishi na maambukizi, wanawake 222 na Wanaume 138.

"Hawa watu wawili tuliowagundua wameisha ingizwa katika mfumo wa kupata Dawa (ARVs) na wanaendelea na maisha Yao na tuna wenza 27 ambao Mmoja anamaambukizi na Mwingine hana maambukizi na wanaishi vizuri na kupata watoto bila shaka yoyote" anasema Calen .

Dkt. Godlove Kanyonga kutoka MTI kitengo Cha Afya ya akili na Utengemao amekiri kuwepo Kwa Unyanyapaa Kwa watu wanaoishi na maambukizi ya VVU jambo linalowapa msongo wa mawazo waathiriwa hao.


Wakimbizi wanaoishi na Virusi vya  UKIMWI katika kambi ya Nduta,wilayani Kibondo Mkoani Kigoma wakiwa katika maadhisho ya siku ya UKIMWI Kambini hapo.

" Unyanyapaa upo wa aina mbili Kwa muhusika na wa jamii,Muhusika asipojikubali na ali aliyonayo anajinyanyapaa hivyo anapata msongo wa mawazo ,Lakini upande wa pili jamii ikiwanyanyapaa hawa watu wanapata pia msongo wa mawazo (sonona ) wanafikia hata Hatua ya kufanya maamuzi yasiyo sahihi" amesema Dkt Kanyonga.

Kutokana na hali hiyo wizara ya mambo ya ndani idara ya wakimbizi ofisi ya mkuu wa kambi ya wakimbizi ya Nduta imetoa wito kwa Mashirika yote yanayohudumia wakimbizi kurejea mipango yake ya huduma kwa wakimbizi wenye mahitaji maalumu

Rai hiyo imetolewa na Bw. Iddy Omary Mahuna ambaye ni afisa afya ya jamii kutoka katika ofisi ya mkuu wa kabi ya wakimbizi ya Nduta akielekeza Mashirika kupunguza bajeti za machapisho hususani fulana na kofia wakati wa maadhimisho mbalimbali na pesa hizo zitumike kuwapa huduma walemavu na wenye virusi vya Ukimwi

Kaimu Mganga mkuu wa Wilaya Dkt Frederick Kilindo aliyekuwa mgeni rasmi akijibu Risala ya watu wanaoshina virusi vya UKIMWI amesema mtu anayefanya unyanyapaa kwa Mtu anayeishi na VVU akibainika anaweza kufungwa jela mwa Mmoja au kupigwa faini.

"Kwa mujibu wa Sheria ya UKIMWI ya mwaka 2008 ukimnyanyapaa mtu mwenye UKIMWI unaweza kupigwa faini ya Shilingi Milioni 2 au Kifungo Cha mwaka 1 jela na nadhani tutekeleze hii Sheria" ansema Dkt Kilindo.

Baadhi ya Wakimbizi walioshiriki sherehe hizo akiwemo Mhera Kolonari, amesema wamefurahishwa na siku hiyo Kwani wamepata Elimu kuhusu UKIMWI na kupima bure.

Mwandishi: Harieth Dominick 

Mhariri:Prosper Kwigize

Post a Comment

0 Comments