Mwenyekiti wa Ngome ya
vijana wa ACT Wazalendo Abdul Omary Nondo amepatikana usiku wa kuamkia leo katika
fukwe za Coco beach zilizopo katika bahari ya Hindi jijini Dar es salaam.
Akitoa taarifa hiyo usiku
huo Makamo Mwenyekiti Bara wa chama cha ACT Wazalendo Isihaka Mchinjata amesema
Abdul Nondo alitupwa katika fukwe hizo na kusaidiwa na wasamaria wema ambao walimpeleka
katika ofisi za cha cha ACT Wazalendo zilizopo Kinondoni jijini Dar es salaam.
Mchinjata amesema hali
ya Abdul Nondo ni mbaya kwasababu amepigwa sana katika maeneo mbalimbali ya
mwili wake.
Amesema kwa sasa bado hawana
taarifa zaidi juu ya tukio hilo japo mhanga amepatikana lakini kutokana na hali
aliyokutwa nayo hajaweza kujieleza zaidi.
“Hatua ya kwanza ni
kuangali hali aliyonayo hivyo tukalazimika kumuwahisha hospitali ya Agakhan kwa
ajli ya kupatiwa matibabu, maana alikuwa na maumivu makali karibia mwili mzima,”
amesema Mchinjati.
Aidha ameeleza namna
ambavyo taarifa ziliwafikia kuwa ni baada ya kupigiwa simu na watu waliokuwepo
wakati wa tukio majira ya asubuhi katika Stendi ya mabasi ya Magufuli baada ya
kuokota begi lenye nguo za ACT Wazalendo.
“Tukio lilipotokea
watu walioshuhudia kurupushani wakati wa utekeji waliokota begi lenye nguo za
ACT Wazalendo ndipo wakampigia simu John Mnyika na ufuatiliaji ukaanza haraka
uzuri namba za gari lililotumika zilipatikana,” amesema Mchinjata.
Abdul Nondo ni Mwenyekiti
wa Ngome ya vijana wa ACT Wazalendo jana alitekwa na watu
wasiojulikana baada ya kushuka kwenye basi akitokea mkoani Kigoma, tukio hilo ni
muendelezo wa matukio ya utekaji yanayoendelea hapa nchini kwa siku za hivi
karibuni.
Muandishi: Mussa Mkilanya.
0 Comments