Moja ya maazimio hayo ni kuendeleza Teknolojia za
Matumizi bora ya Nishati ili kuwa na ufanisi katika matumizi ya
nishati hiyo.
Mkutano huo uliokuwa ukifanyika jijini
Arusha Disemba 4-5 mwaka huu umefungwa na Waziri wa Viwanda na Biashara, Dkt.
Selemani Jafo ambaye ameeleza kuwa umehusisha Watunga Sera,
Sheria, Viongozi, Wataalam na Wabobezi katika masuala ya Nishati kwa
lengo moja la kuwa na matumizi sahihi ya Nishati.
Dkt. Jafo amesema lengo la nchi ni kuendelea
kukuza uchumi, viwanda vifanye kazi na biashara zifanyike kwa ufanisi
lakini hilo litawezekana ikiwa kuna nishati ya kutosha ambayo uwepo wake
unategemea usahihi katika matumizi yake.
Ameeleza kuwa, Tanzania inatilia mkazo suala la
matumizi bora ya
nishati ambapo kwa sasa Shirika la Viwango
Tanzania (TBS) linaandaa viwango fanisi vya vifaa vya nishati
vinavyozalishwa au kuingizwa nchi ambavyo vitawezesha nchi kutumia umeme kwa ufanisi.
Amemshukuru Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa
kuendelea kuwekeza katika miradi ya Nishati ambapo uwekezaji huo
amesema kwamba una maana kubwa katika kuendeleza viwanda na
biashara.
Waziri wa Viwanda na Biashara, Dkt. Selemani Jafo akiwa katika picha ya pamoja na Menejimenti ya Wizara ya Nishati, wakati akifunga Mkutano wa Kikanda wa Matumizi Bora ya Nishati uliofanyika Arusha.
Aidha, ameishukuru Wizara ya Nishati kwa kuratibu
Mkutano huo wa Siku mbili kwa kushirikiana na Umoja wa Ulaya (EU),
Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) na Ubalozi wa Ireland.
Kwa upande wake, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya
Nishati, Dkt. Khatibu Kazungu amesema Serikali ya Tanzania kupitia
Wizara ya Nishati imejipanga kutekeleza Mkakati wa Matumizi Bora ya Nishati uliozinduliwa tarehe 4 Desemba 2024 kwa
kuhakikisha Mkakati huo unatekelezwa kwa kuwekewa bajeti ili nchi iweze
kuwa na ufanisi katika vifaa vya nishati.
Amesema kupitia Mkutano wa REEC 2024 maazimio
mbalimbali yamefikiwa ikiwemo kufanya tafiti za pamoja ili kuboresha
matumizi bora ya nishati na kuihusisha kikamilifu Sekta Binafsi.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya
Bunge ya
Miundombinu, Mhe.Selemani Kakoso amsipongeza
Serikali kwa kuendesha na kusimamia mkutano wa REEC 2024 ulioleta
mafanikio makubwa ikiwemo mafunzo na kubadilishana uzoefu ili kuwa
na ufanisi.kwenye matumizi ya nishati.
Mwandishi: Na Mwandishi wetu.
0 Comments