Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Hussein Ali Mwinyi
ametunukiwa Shahada ya Heshima ya
Uzamivu ya Chuo Kikuu cha Zanzibar.
Chuo Kikuu cha Zanzibar kimemtunuku Shahada hiyo ikiwa ni kutambua na kuthamini Mchango wa Uongozi wake Unaoacha Alama na historia itakayokumbukwa wakati wote.
Hafla ya kutunukiwa Shahada hiyo imefanyika leo tarehe
5 Disemba 2024 katika Viwanja vya Chuo Kikuu cha Zanzibar Tunguu wakati wa
Mahafali ya 22 ya Wahitimu wa mwaka 2024
Shahada hiyo ya Heshima ya Uchumi ametunukiwa kuthamini Mchango wake na
Mafanikio makubwa yaliofikiwa Zanzibar hususan
Ukuaji wa Uchumi na Maendeleo
yaliopatikana Kipindi kifupi cha Uongozi wake wa miaka minne akiwa Rais wa
Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi.
Rais Dkt. Mwinyi amekishukuru Chuo hicho kwa kuthamini
juhudi na kazi anazofanya kwa ajili ya Maendeleo ya nchi.
Aidha Rais Dkt.Mwinyi
amebainisha kuwa Shahada hiyo
aliotunukiwa Inaakisi kazi nzuri inayoifanya na Serikali anayoiongoza na
itamuongezea hamasa ya kufanya Maendeleo zaidi.
Na Mwandishi wetu.
0 Comments