Uamuzi wa kuwafukuza wanafunzi haukufuata utaratibu wamerudishwa.

 


Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Nkasi, Afraha Hassan amesema wanafunzi waliofukuzwa shule kwa madai kuwa wazazi wao ni wafuasi wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA wamerudishwa shuleni.

Akitoa taarifa hiyo leo Mkurugenzi huyo amesema wanafuzi waliokutwa na Mkasa huo walikuwa tisa na tayari wamewarudisha muda mfupi tangu taarifa ya kufukuzwa kwa wanafunzi hao wa Shule ya Msingi Izinga kusambaa mitandaoni.

Kwa mujibu wa Taarifa hiyo ya Mkurugenzi imesema wamebaini kuwa Mwalimu Mkuu aliwasimamisha shule wanafunzi hao na kuwataka wazazi watafute shule nyingine na siyo kufukuzwa shule kama ilivyoripotiwa katika mitandao mbalimbali ya kijamii.

“Uamuzi wa kuwasimamisha wanafunzi hao haukufuata utaratibu wa miongozo ya wizara. Aidha wanafunzi waliosimamishwa shule hawakuwa na kosa lolote la kinidhamu,” amesema Mkurugenzi.

Aidha Mkurugenzi amesema hatua za kiutawala na uongozi dhidi ya Mwalimu Mkuu wa shule hiyo zitachukuliwa pindi uchunguzi unaoendelea utapokamilika.

Mapema leo asubuhi, Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia, Profesa Adolf Mkenda aliagiza timu ya wataalamu udhibiti ubora kwenda kuchunguza taarifa ya wanafunzi hao wa Shule ya Msingi Izinga, iliyopo Nkasi Kusini kufukuzwa shule kwa madai ya wazazi wao kuipigia kura CHADEMA katika uchaguzi wa serikali za mitaaa uliofanyika Novemba 27 mwaka huu.

Muandishi: Mussa Mkilanya.

Post a Comment

0 Comments