Mkuu wa Wilaya Kasulu atoa agizo Kupandisha ufaulu shule za Msingi

Mkuu wa wilaya ya kasulu Kanali Isaac Mwakisu ameeleza kutoridhishwa na usimamizi wa Elimu na matokeo ya shule za Msingi katika Halmashauri ya Mji Kasulu baada ya kushika nafasi ya 6 matokeo darasa la 7 kimkoa kati ya Halmashauri 8 za Mkoa wa Kigoma.

Akizungumza Decemba 11 katika kikao cha baraza la madiwani la halmshauri ya mji Kasulu Kanalii Mwakisu ametoa maagizo kwa mkurugenzi na afisa elimu wa halmashauri hiyo kuhakikisha wanafuatilia na kubaini sababu za kiwango cha Elimu kushuka katika halmshauri hiyo.

“Sasa hivi tumekuwa wa 6 mimi sijaridhishwa na usimamizi wa shule za msingi na matokeo yanavyotokea Afisa elimu sijaridhika na mwenendo wa ufaulu wa idara yako nimefanya utafiti miaka mitatu nyuma kila muda mnashuka viwango nitaanza ukaguzi wa kushtukiza, mkurugenzi nataka uniambie kila shule ina walimu wangapi haiwezekani kila mwaka mnashuka tu hadi mmeshika nafasi ya 6 haiwezekani” Amesema Kanali Mwakisu.

Baadhi ya madiwani wakishiriki baraza la madiwani katika halmashauri ya mji Kasulu

Aidha makamu mwenyekiti wa halmshauri ya mji kasulu bw.Selemani Kwirusha ameeleza kusikitishwa na matokeo ya darasa la 7 na kuwataka madiwani kushirikiana katika kukuza taaluma ya wanafunzi shule za msingi katika halmashauri ya Mji Kasulu.

“Nimeyapokea Matokeo haya kwa masikitiko makubwa, hiki alichokisema mkuu wetu wa wilaya hakijafurahisha mtu yeyote na waheshimiwa Madiwani niwaombe sana kila mtu alichukulie kwa uzito swala hili ni aibu pamoja na mkurugenzi nimuagize kwa umuhimu huu ambavyo umeuchukulia kwa jinsi mlivyojipanga na kabineti yako mje  na visababishi ili tujuwe sababu ni nini” Amesema makamu mwenyekiti wa halmshauri Kwirusha. 

Katika hatua nyingine Mkurugenzi wa halmshauri ya mji kasulu Mwl Vumilia Simbeye amesema wameshaanza ufuatiliaji na kutoa maagizo kwa wakuu wote wa shule za msingi kuhakikisha wanasimamia swala hili ili jitihada za kukuza taaluma ya elimu kwa shule za msingi.

“Matokeo mazuri sisi ndo tutakaosababisha na matokeo mabaya sisi ndo tutasababisha hatuna namna ya kukwepa, kwa kuwa sis indo wasababishi wa matokeo hayo tayari tushafanya tathmini na tumejiona tulipo hakuna ambaye ameridhika na tumeshaanza mikakati ya kuboresha na tunaamini mwakani tutafanya kitu bora tofauti na mwaka huu.

Hata hivyo Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu mkoani Kigoma iling’ara katika matokeo ya darasa la saba 2024 kwa kushika nafasi ya pili kimkoa kati halmashauri nane zilizopo baada ya kupata ufaulu wa 85.6%. 

Mwandishi, Sharfati Shinji

Mhariri, Ramadhani Zaidy

Post a Comment

0 Comments