Waziri Mkuu,
Mhe.Kassim Majaliwa amekemea utaratibu wa uwekaji wa Vizuizi na vituo vya
ukaguzi barabarani bila kuzingazia tahadhari ya usalama kwa watumiaji wengine
wa barabara.
Mhe. Majaliwa amekemea
utaratibu huo leo jijini Arusha wakati akifungua Kongamano la Kimataifa la 14
la Taasisi ya Wahandisi Tanzania (IET), na kusisitiza kuwa mwenye dhamana kutoa
kibali cha kuweka vizuizi na vituo vya ukaguzi ni Jeshi la Polisi.
Amesema hatua hiyo inatokana
na Halmashauri kuwa na utaratibu wa kuweka vizuizi na vituo vya ukaguzi kwa
kuziba barabara bila ya kuzingatia matumizi sahihi ya barabara na hivyo
kusababisha ajali.
“Jeshi la Polisi kaeni
na Halmashauri, vizuizi vyao barabarani vinasababisha ajali, hakuna sababu ya
Halmashauri kuweka kizuizi cha kuzuia magari, mwenye kibali hicho ni Jeshi la
Polisi peke yake kwa ajili ya ukaguzi wa usalama”, amesema Waziri Mkuu
Majaliwa.
Waziri Mkuu ameeleza
kuwa kuna baadhi ya Halmashauri zimeweka vizuizi barabarani kwa ajili maafisa
kukusanya mapato ambapo utaratibu huo umekuwa ukiathiri watumiaji wengine wa
barabara na kusababisha ajali katika maeneo hayo.
Aidha, amewataka
Wahandisi na wataalamu wa miundombinu kuwa kiungo muhimu katika utekelezaji wa
maelekezo hayo kwa kuendelea kutoa mapendekezo ya kitaalamu ya matumizi sahihi
ya barabara ili kuhakikisha kuwa dhamira ya Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu
Hassan ya kuifanya Tanzania kuwa salama zaidi kwa wote inatimia na inapewa
kipaumbele.
Mwandishi: Na Mwandishi wetu.
0 Comments