Makubaliano hayo yamefanyika Desemba 15 wakati Dk Ndumbaro akisikiliza
matatizo na kuzungumza na wafungwa katika Gereza la Kiberege lililipo wilayani
Kilombero mkoani Morogoro kupitia Kampeni ya ‘Mama Samia Legal Aid Campaign’.
Waziri Ndumbaro ameagiza kambi hiyo ianzie kazi mara moja
katika Gereza la Kiberege, ambapo mawakili wa TLS watashiriki kutoa msaada wa
kisheria kwa wafungwa wenye changamoto mbalimbali za kisheria.
Wakati wa zoezi hilo, Waziri Dk Ndumbaro ametoa msaada wa kisheria kwa wafungwa 15 na mahabusu wawili na amesisitiza kuwa serikali itaendelea kuhakikisha haki inapatikana kwa wafungwa na mahabusu wote, hususan wale waliofungwa kwa makosa ya kusingiziwa.
Kwa upande baadhi ya wafungwa katika gereza la Kiberege mkoani Morogoro wameeleza kufurahishwa na utaratibu na kampeni hiyo ya ‘Mama Samia Legal Aid Campaign’ ambayo utawasaidia kutambua haki zao za kimsingi kwa mujibu wa katiba na sheria.
Huku Lengo kuu la Kampeni ni ni kulinda na kukuza
upatikanaji wa haki kwa wote kupitia huduma ya msaada wa kisheria nchini.
Mwandishi: Ramadhani Zaidy
0 Comments