Mbunge na Waziri wa nchi Offisi ya rais pro.kitila Mkumbo ametangaza nia kugombea tena ubunge



Mbunge wa Ubungo na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, Profesa Kitila Mkumbo, ametangaza nia yake ya kugombea tena ubunge wa jimbo hilo katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 huku akiwaonya watu aliowaita wanafiki.

Akizungumza Jumatano Januari 1, 2025 katika hafla ya Fungua Day, ameweka wazi msimamo wake dhidi ya watu wanaojifanya kumuunga mkono huku wakishirikiana na wapinzani wake kisiasa.

“Hakuna boya hata moja kwangu, nawaambia wapigakura wangu msidhani kwamba nyoka mdogo hana sumu. Sumu ni ileile, haijalishi ukubwa wa nyoka,” amesema Profesa Mkumbo.

Akionyesha dhamira yake ya kuendelea kutumikia wananchi wa Ubungo, Profesa Mkumbo amesema: “Mungu akijalia afya njema, nitagombea tena 2025. Nimejipanga zaidi ya 2020, na siasa si mahali pa kuhubiri mbinguni. Katika siasa unambeba anayekubeba, anayekutupa unamtupa,” amesema.

Na mwandishi wetu 

Mhariri:Abel  Mahenge 


Post a Comment

0 Comments