Radi imeua ng’ombe 16 katika Kijiji cha Ngolotwa, wilayani Kalambo, mkoani Rukwa



Tukio hilo limetokea Jumatano Januari 1, 2025 wakati ng’ombe hao wakichungwa katika hifadhi ya Kalambo mkoani humo, huku mmiliki mpaka sasa akiwa hajafahamika.

Mhifadhi Mkuu wa Wilaya ya Kalambo, Ibrahim Mkiwa amesema wamewakuta ng’ombe hao wamekufa hifadhini humo, huku akitoa rai kwa wananchi kutoingiza mifugo hifadhini.

Mganga Mkuu wa mifugo wilayani humo, Dk Ennosy Luvinga amesema baada ya uchunguzi wamebaini ng’ombe hao wamekufa kwa kupigwa na radi.

Hili ni tukio la pili mfululizo kwa mifugo kufa kwa kupigwa na radi mkoani humo, ambapo la kwanza lilitokea Desemba 9, 2024 baada ya ng'ombe 22 kupigwa radi wakiwa zizini katika Kijiji cha Songambele Kata ya Azimio wilayani Sumbawanga.


Na mwandishi wetu 

Mhariri : Abel Mahenge 

Post a Comment

0 Comments