Baraza la Mitihani la Tanzania (Necta) limetangaza matokeo ya upimaji wa kitaifa wa kidato cha nne na kusema ufaulu umeongezeka kwa asiliimia 3 na kufikia asilimia 92.37 ukilinganisha na ufaulu wa mwaka 2023.
Matokeo hayo yametangazwa leo
Alhamisi na Katibu Mtendaji wa Necta, Dk Said Mohammed jijini DaresSalaam
ambapo Jumla ya watahiniwa wa shule 477,262 kati ya 516,695 wenye matokeo ambao
ni sawa na asilimia 92.37 wamefaulu ambapo wamepata madaraja ya I, II, III na
IV.
Said, umeongezeka kwa kusema Ubora wa ufaulu wa Madaraja ya Kwanza mpaka tatu ni mzuri zaidi kwa kundi la wavulana, ikilinganishwa na Wasichana, ambapo Wavulana ni 119,869 sawa na asilimia 48.90 ya Wavulana wote, huku Wasichana wakiwa 102,084 sawa na asilimia 37.59 ya Wasichana wote
"Matokeo ya kidato cha nne 2024 takwimu zinaonyesha kuwa ufaulu wa jumla
umepanda kwa asilimia 3, na hivyo kufikia asilimia 92.37 ambapo watahiniwa laki
nne sabini na saba elfu mia mbili sitini na mbili, kati ya watahiniwa laki tano
kumi na sita elfu mia sita tisini na tano, kwenye matokeo wamefaulu kwa kupata
madaraja ya kwanza, pili, tatu na nne."
Pia Baraza hilo la Mitihani la Tanzania limefuta matokeo ya wanafunzi 67
waliofanya udanganyifu na wanafunzi 5 walioandika matusi kwenye karatasi za
kujibia huku likizuia matokeo ya
wanafunzi 459 kwa sababu mbalimbali zilizosababisha wasifanye mitihani yote
zikiwemo matatizo ya kiafya na baraza liokitoa nafasi ya kurudia mitihani
kwawanafunzi hao mwaka 2025
Mwandishi wetu.
Mhariri Paul Masanja
0 Comments