Mh Noel Hanula
amesema hayo leo januari 22, 2025 katika ukumbi wa halmashauri ya mji kasulu
wakati wakikabidhi pesa hizo za mikopo kwa wanawake hao na kusema kuwa lengo la
serikali ni kuhakikisha mkopo huo unatumiwa katika malengo yaliotumika kuomba
mkopo huo.
“mikopo hii umetolewa na mh Rais kwa lengo la kujikwamua kiuchumi kwa kuwa awali ilisitishwa kutokana na wanifaika kutumia kinyume na malengo hivyo niwaombe mama zangu tutumie mikopo hii kwa lengo la kujikwamua kiuchumi kama dhamira ya Rais Samia na kutumia kwa matumizi yetu binafsi” amesema Mwenyekiti wa halmashauri ya mji Kasulu na diwani wa kata ya heru juu Noel Hanula.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa halmashauri ya Kasulu Mji Mwalimu Vumilia Simbeye amewasisitiza
wanawake hao kuhakikisha wananza marejesho ya mikopo hiyo kwa wakati kama
walivyokubaliana ili kuepusha usumbufu kwa serikali kwani riba imeondolewa kwa
lengo la kurahusisha ulipaji wa mikopo hiyo.
“wananchi wote
inabidi watambue kwamba mikopo hii haina riba na ni nafuu kwa wananchi wa
wananufaika hivyo basi nitoe wito kwa wananchi waliochukua mikopo hii kurudisha
katika muda ulipangwa ili na wengine wanufaike kwa sababu tumeona haja ya kutoa
riba katika mikopo hii ili urejeshwaji wake uwe rahisi kwao” amesema Mkurugenzi
wa halmashauri ya Kasulu Mji Mwalimu Vumilia Simbeye.
Nao baadhi wanufaika
wa mikopo kutoka katika vikundi mbalimbali ambavyo leo vimepata mikopo hiyo
wameahidi kutekeleza kule kilichoainishwa katika makubaliano ya awali kabla kuchukua
mikopo hiyo kwa ajili ya kuinua uchumu kwa kundi husika na kurejesha mikopo
hiyo kwa wakati.
0 Comments