Huduma ya msaada wa sheria wa mama Samia yaleta tija Kasulu

 Kampeini ya msaada wa kisheria ya Samia legal aid imefanikiwa kutatua mgogoro  wa ardhi uliodumu kwa mwaka Moja katika kata ya kulugongo

Mgogoro huo uliokuwa ukilalamikiwa na bi Angelina Kadakila kuhusu ardhi iliyouzwa na mme wake Yassin Jonas  bila kumshirikisha mke wake kwa Debora Danford  ambae amekubali kulipa fidia ya garama ya lakisita 

Mara Baada ya kupatika a suluhu hio wananchi hao wameshukuru ujio wa msaada huo wa kisheria kwani umewaepusha kutumia garama nyingi  kwenda kutafuta haki na na kuepusha mgogoro baina Yao

Bw. Moses Basila mratibu wa kampeni akitoa huduma ya msaada wa sheria kwa wananchi wilayani Kasulu

Mratibu wa kampeini hio ya msaada wa kisheria halmashauri ya wilaya kasulu Moses basila amesema katika kata ya kulugongo wamebaini uwepo wa migogoro mingi ya ndoa inayopelekea kujimilikisha Mali na ukatili wa kijinsia unaopelekea kukosekana kwa malezi ya watoto

Ameongeza kuwa kupitia msaada huo wa kisheria wa Samia legal aid  lengo kubwa ni kutatua changamoto za migogoro na kufikia makubaliano kwa njia ya majadiliano  kama ilivyofanyika kwa bi Angelina na Debora

Mwandishi: Paul Masanja, Buha News

Post a Comment

0 Comments