Jamii Yaonywa kuhusu unyanyapaa na Ukatili kwa Watoto

 


Utafiti Tatuzi kuhusu Elimu Jumuishi wazinduliwa Kigoma,  

Wananchi katika Halmashauri ya Mji Kasulu Mkoani Kigoma wameombwa kutojihusisha na vitendo vya Unyanyapaa kwa Watu wenye Ulemavu pamoja na kutojihusisha katika vitendo vya  ukatili kwa watoto waliopo shuleni  ili Kujenga  usitawi na maendeleo bora katika jamii.

Hayo yamesemwa leo na  Kamishna wa Elimu Tanzania Dkt. Lyabwene Mtahabwa wakati akizungumza katika Hafula ya  Kongamano la uzinduzi wa program ya utafiti tatuzi kuhusu Usalama Jumuishi katika Elimu lililofanyika katika Kiwanja cha Mpira Kiganamo na kusisitiza jamii inawalinda watoto wote wenye ulemavu na wasio na ulemavu ili kujenga jamii bora.

“Naomba kila kiongozi wa Tanzania kuanzia ngazi za serikali za mitaa hadi ngazi ya taifa utendaji wake uanze kwa kuangalia  ni kwa namna gani anasimamia kwa dhati usalama, ustawi na maendeleo ya watoto, kama wewe  ni kiongozi wa kimila, kidini, kiselikali lazima uzingatie usalama, ustawi na maendeleo ya  watoto” Amesema DKT. Mtahabwa. 

Kamishna wa Elimu Tanzania Dkt. Lyabwene Mtahabwa

Aidha Dkt. Mtahabwa amesema watu wote wanaojihusisha na kuwanyanyasa  na kusababisha kukosekana kwa usalama, ustawi  na maendeleo ya motto atachukuliwa hatua kali za kisharia ili kuhakikisha anakuwa mfano kwa watu waote watakaokiuka taratibu hizo.

“ Mtu yeyote atakayesababisha  hatari ya usalama ,ustawi na maendeleo ya motto kwa makusudi hatutosita kumchukulia kupambana nae kwa njia zote na kumchukulia hatua kinidham na  za kisheria sisi tunataka watoto wajisikie furaha, amani wawapo njiani, nyumbani, au shileni” Amesema  Dkt. Mtahabwa

Awali Kaimu Katibu Tawala mkoa wa kigoma Bi. Paulina Ndigeza ameshukuru na kumpongeza Dkt.  Lyabwene Mtahabwa  kuwa mgeni rasimi katika Hafla hiyo na kusema Mkoa wa kigoma inao watoto wanaosoma katika shule jumuishi huku akiahidi mkoa wa kigoma na mikoa mingine mitatu iliyoteuliwa kufanya utafti huo kuwa wataufanyia kazi vizuri.

“Kwanza nikupongeze kwa kukubali mwaliko huu wa kuja kuwa mgeni rasmi katika hafla hii na umejionea mengi yaliyooneshwa  na watoto mbele yako hapa  mkoa wa kigoma ni miongoni mwa mikoa mine iliyoteuliwa kufanya utafti huu na kama ulivyoona tunao watoto wanaosoma katika shule jumuishi umeona ushuda wa mwanafunzi  aliyekuja kutoa ushuda kutoka shule ya Sekondari Kigama Grand hivyo tukuahidi tu tutaenda kulifanyia kazi hili” Amesema  Bi. Ndigeza.

Mwalimu Paulina Ndigeza (katikati) Kaimu Katibu tawala mkoa wa Kigoma ambaye pia ni Afisa Elimu Mkoa


Katika hatua nyingine Ndize Juma ambaye ni mwanafunzi mwenye ulemavu kutoka shule ya Sekondari Kigoma Grand amesema wananchi na jamii kwa ujumla  wanapaswa kuacha tabia ya kuwanyanyapaa watu wenye ulemavu hasa katika swala la elimu.

Mpango wa Programu ya Utafiti Tatuzi Kuhusu Usalama Jumuishi katika Elimu umezinduliwa leo chini ya taasisi ya Elimu Bora nchini ikiwa na lengo la kuwasaidiwa watoto wote nchini wenye ulemavu na wasio na ulemavu wanapata elimu bora bila changamoto yoyote ya unyanyapaa pamoja na ukatili juu yao.

Imeandikwa na Sharifat Shinji


Post a Comment

0 Comments